1 Ee Bwana, unihukumu mimi, Maana nimekwenda kwa ukamilifu wangu, Nami nimemtumaini Bwana bila wasiwasi.
Psaumes 7.8 2 Rois 20.3 Psaumes 28.7 Proverbes 20.7 Hébreux 10.23
2 Ee Bwana, unijaribu na kunipima; Unisafishe mtima wangu na moyo wangu.
Psaumes 7.9 Psaumes 17.3 Job 31.4-31.6 Jérémie 20.12 Psaumes 139.23-139.24
3 Maana fadhili zako zi mbele ya macho yangu, Nami nimekwenda katika kweli yako.
2 Rois 20.3 Esaïe 2.5 Jean 14.6 Ephésiens 4.32-5.2 Psaumes 85.10-85.13
4 Sikuketi pamoja na watu wa ubatili, Wala sitaingia mnamo wanafiki.
Psaumes 1.1 Psaumes 119.115 Jérémie 15.17 Proverbes 9.6 Proverbes 12.11
5 Nimelichukia kusanyiko la watenda mabaya, Wala sitaketi pamoja na watu waovu.
Psaumes 31.6 Psaumes 139.21-139.22 Psaumes 101.3-101.8 1 Corinthiens 5.9-5.11 Psaumes 1.1
6 Nitanawa mikono yangu kwa kutokuwa na hatia, Na kuizunguka madhabahu yako, Ee Bwana
Psaumes 73.13 Exode 30.19-30.20 Psaumes 43.4 Hébreux 10.19-10.22 Psaumes 24.4
7 Ili niitangaze sauti ya kushukuru, Na kuzisimulia kazi zako za ajabu.
Psaumes 9.1 Psaumes 72.18 1 Samuel 1.27 Psaumes 95.2 Psaumes 116.18-116.19
8 Bwana, nimependa makao ya nyumba yako, Na mahali pa maskani ya utukufu wako.
Luc 2.49 Jean 2.14-2.17 1 Chroniques 29.3 Luc 19.45-19.47 Exode 40.34-40.35
9 Usiiondoe nafsi yangu pamoja na wakosaji, Wala uhai wangu pamoja na watu wa damu.
Psaumes 139.19 1 Samuel 22.18-22.19 1 Samuel 25.29 Matthieu 25.32 Malachie 3.18
10 Mikononi mwao mna madhara, Na mkono wao wa kuume umejaa rushwa.1 Samuel 8.3 Exode 23.8 Deutéronome 16.19 Actes 23.12 Psaumes 52.2
11 Ila mimi nitakwenda kwa ukamilifu wangu; Unikomboe, unifanyie fadhili.
Psaumes 69.18 Psaumes 26.1 Tite 2.14 Psaumes 103.7-103.8 Job 1.1
12 Mguu wangu umesimama palipo sawa; Katika makusanyiko nitamhimidi Bwana.
Psaumes 27.11 Psaumes 40.2 Proverbes 10.9 Psaumes 111.1 Psaumes 122.4