1 Ee Bwana, unihukumu mimi, Maana nimekwenda kwa ukamilifu wangu, Nami nimemtumaini Bwana bila wasiwasi.
Psaumes 7.8 Psaumes 28.7 Proverbes 20.7 2 Rois 20.3 Psaumes 4.5
2 Ee Bwana, unijaribu na kunipima; Unisafishe mtima wangu na moyo wangu.
Psaumes 7.9 Psaumes 17.3 Job 31.4-31.6 Jérémie 20.12 Psaumes 139.23-139.24
3 Maana fadhili zako zi mbele ya macho yangu, Nami nimekwenda katika kweli yako.
2 Rois 20.3 Matthieu 5.44-5.48 Luc 6.36 2 Corinthiens 5.14-5.15 3 Jean 1.3-1.4
4 Sikuketi pamoja na watu wa ubatili, Wala sitaingia mnamo wanafiki.
Psaumes 1.1 Psaumes 119.115 Jérémie 15.17 Proverbes 9.6 Proverbes 12.11
5 Nimelichukia kusanyiko la watenda mabaya, Wala sitaketi pamoja na watu waovu.
Psaumes 31.6 Psaumes 139.21-139.22 Psaumes 101.3-101.8 1 Corinthiens 5.9-5.11 Psaumes 1.1
6 Nitanawa mikono yangu kwa kutokuwa na hatia, Na kuizunguka madhabahu yako, Ee Bwana
Psaumes 73.13 Exode 30.19-30.20 Psaumes 43.4 Hébreux 10.19-10.22 Psaumes 24.4
7 Ili niitangaze sauti ya kushukuru, Na kuzisimulia kazi zako za ajabu.
Psaumes 9.1 Psaumes 118.19 Psaumes 136.4-136.5 Psaumes 9.14 Psaumes 105.2
8 Bwana, nimependa makao ya nyumba yako, Na mahali pa maskani ya utukufu wako.
Luc 2.49 Jean 2.14-2.17 2 Chroniques 5.14-6.2 Exode 25.21-25.22 Psaumes 122.1-122.4
9 Usiiondoe nafsi yangu pamoja na wakosaji, Wala uhai wangu pamoja na watu wa damu.
Psaumes 139.19 Matthieu 25.32 Malachie 3.18 Psaumes 28.1-28.3 Matthieu 24.51
10 Mikononi mwao mna madhara, Na mkono wao wa kuume umejaa rushwa.
Deutéronome 16.19 1 Samuel 8.3 Exode 23.8 Esaïe 33.15 Psaumes 36.4
11 Ila mimi nitakwenda kwa ukamilifu wangu; Unikomboe, unifanyie fadhili.
Psaumes 69.18 Psaumes 26.1 1 Thessaloniciens 2.10 Néhémie 13.22 Psaumes 103.3-103.4
12 Mguu wangu umesimama palipo sawa; Katika makusanyiko nitamhimidi Bwana.
Psaumes 27.11 Psaumes 40.2 Proverbes 10.9 Psaumes 111.1 Psaumes 122.4