Prière de l’homme intègre
1 Ee Bwana, unihukumu mimi, Maana nimekwenda kwa ukamilifu wangu, Nami nimemtumaini Bwana bila wasiwasi.
Psaumes 7.8 Psaumes 28.7 Proverbes 20.7 2 Rois 20.3 1 Corinthiens 4.3-4.6
2 Ee Bwana, unijaribu na kunipima; Unisafishe mtima wangu na moyo wangu.
Psaumes 7.9 Psaumes 17.3 Job 31.4-31.6 Jérémie 20.12 Psaumes 139.23-139.24
3 Maana fadhili zako zi mbele ya macho yangu, Nami nimekwenda katika kweli yako.
2 Rois 20.3 Psaumes 25.5 Psaumes 101.2 Psaumes 52.1 2 Corinthiens 8.9
4 Sikuketi pamoja na watu wa ubatili, Wala sitaingia mnamo wanafiki.
Psaumes 1.1 Psaumes 119.115 Jérémie 15.17 Proverbes 13.20 Proverbes 9.6
5 Nimelichukia kusanyiko la watenda mabaya, Wala sitaketi pamoja na watu waovu.Psaumes 31.6 Psaumes 139.21-139.22 Psaumes 101.3-101.8 1 Corinthiens 5.9-5.11 Psaumes 1.1
6 Nitanawa mikono yangu kwa kutokuwa na hatia, Na kuizunguka madhabahu yako, Ee Bwana
Psaumes 73.13 Psaumes 43.4 Exode 30.19-30.20 Tite 3.5 Malachie 2.11-2.13
7 Ili niitangaze sauti ya kushukuru, Na kuzisimulia kazi zako za ajabu.
Psaumes 9.1 Psaumes 100.4-100.5 Psaumes 116.12-116.14 Psaumes 66.13-66.15 Psaumes 134.2
8 Bwana, nimependa makao ya nyumba yako, Na mahali pa maskani ya utukufu wako.
Luc 2.49 Jean 2.14-2.17 Esaïe 38.22 Psaumes 84.10 Psaumes 84.1-84.2
9 Usiiondoe nafsi yangu pamoja na wakosaji, Wala uhai wangu pamoja na watu wa damu.
Psaumes 139.19 Psaumes 55.23 2 Samuel 21.1 2 Samuel 16.7 Matthieu 25.44
10 Mikononi mwao mna madhara, Na mkono wao wa kuume umejaa rushwa.
1 Samuel 8.3 Exode 23.8 Deutéronome 16.19 Amos 5.12 Proverbes 1.16
11 Ila mimi nitakwenda kwa ukamilifu wangu; Unikomboe, unifanyie fadhili.
Psaumes 69.18 Psaumes 26.1 Psaumes 49.7 1 Pierre 1.18-1.19 Néhémie 13.31
12 Mguu wangu umesimama palipo sawa; Katika makusanyiko nitamhimidi Bwana.
Psaumes 27.11 Psaumes 40.2 Psaumes 111.1 Proverbes 10.9 Psaumes 22.22-22.25