1 Kwa sauti yangu nitamlilia Bwana, Kwa sauti yangu nitamwomba Bwana dua.
Psaumes 30.8 Psaumes 57.1 Psaumes 54.1 Psaumes 141.1 Psaumes 28.2
2 Nitafunua mbele zake malalamiko yangu, Shida yangu nitaitangaza mbele zake.
Esaïe 26.16 Hébreux 5.7 Romains 8.26 Psaumes 102.1-102.28 Philippiens 4.6-4.7
3 Nilipozimia roho uliyajua mapito yangu; Katika njia niendayo wamenifichia mtego.
Psaumes 140.5 Psaumes 143.4 Psaumes 1.6 Psaumes 141.9 Psaumes 139.2-139.4
4 Utazame mkono wa kuume ukaone, Kwa maana sina mtu anijuaye. Makimbilio yamenipotea, Hakuna wa kunitunza roho.
Psaumes 31.11 Psaumes 88.8 Psaumes 88.18 Psaumes 69.20 Jérémie 30.17
5 Bwana, nimekuita nikasema, Ndiwe kimbilio langu, Fungu langu katika nchi ya walio hai.
Psaumes 16.5 Psaumes 27.13 Psaumes 46.1 Lamentations 3.24 2 Timothée 4.17
6 Ukisikilize kilio changu, Kwa maana nimedhilika sana. Uniponye nao wanaonifuatia, Kwa maana wao ni hodari kuliko mimi.
Psaumes 79.8 Psaumes 116.6 Psaumes 17.1 Psaumes 3.1 Psaumes 18.17
7 Uitoe nafsi yangu kifungoni. Nipate kulishukuru jina lako. Wenye haki watanizunguka, Kwa kuwa Wewe unanikirimu.
Psaumes 13.6 Psaumes 143.11 Psaumes 146.7 Psaumes 116.7 Jacques 5.11