Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 43
Bible en Swahili de l’est


Attente de l’intervention divine

1 Ee Bwana, unihukumu, unitetee kwa taifa lisilo haki, Uniokoe na mtu wa hila asiye haki.
1 Samuel 24.15 Psaumes 26.1 Psaumes 35.1 Psaumes 5.6 Psaumes 35.24
2 Kwa kuwa Wewe ndiwe Mungu uliye nguvu zangu; kwa nini umenitupa? Kwa nini ninakwenda nikihuzunika, adui wakinionea?
Psaumes 42.9 Psaumes 28.7 Psaumes 44.9 Exode 15.2 1 Chroniques 28.9
3 Niletewe nuru yako na kweli yako ziniongoze, Zinifikishe kwenye mlima wako mtakatifu na hata maskani yako.
Psaumes 2.6 Psaumes 84.1 Psaumes 40.11 Psaumes 3.4 Jean 1.17
4 Hivyo nitakwenda madhabahuni kwa Mungu, kwa Mungu aliye furaha yangu na shangwe yangu; Nitakusifu kwa kinubi, Ee MUNGU, Mungu wangu.
Psaumes 57.8 Habakuk 3.17-3.18 Psaumes 81.2 Romains 5.11 Psaumes 42.6
5 Nafsi yangu, kwa nini kuinama, Na kufadhaika ndani yangu? Umtumaini Mungu; Kwa maana nitakuja kumsifu, Aliye afya ya uso wangu, Na Mungu wangu.
Psaumes 42.5 Psaumes 42.11

Cette Bible est dans le domaine public.