Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Job 35
Bible en Swahili de l’est


Appel à rechercher Dieu

1 Tena Elihu akajibu na kusema,
2 Je! Wewe wadhani kwamba haya ni haki yako, Au je! Wasema, Haki yangu ni zaidi kuliko ya Mungu,
Matthieu 12.36-12.37 Job 40.8 Job 27.2-27.6 Job 16.17 Luc 19.22
3 Maana wasema, Kutakuwa na faida gani kwako wewe? Tena, Nitapata faida gani, kuliko nikifanya dhambi?
Job 34.9 Job 9.30-9.31 Malachie 3.14 Job 9.21-9.22 Psaumes 73.13
4 Mimi nitakujibu, Na hawa wenzio pamoja nawe.
Job 34.8 Proverbes 13.20
5 Ziangalie mbingu ukaone; Na mawingu yaangalie, yaliyo juu kuliko wewe.
Job 22.12 Nahum 1.3 Esaïe 55.9 Esaïe 40.22-40.23 Job 37.16
6 Ikiwa umefanya dhambi, umefanya nini juu yake? Yakiwa makosa yako yameongezeka, wamfanyia nini yeye?
Proverbes 8.36 Jérémie 7.19 Proverbes 9.12
7 Ikiwa u mwenye haki, wampa kitu gani? Au yeye hupokea nini mkononi mwako?
Job 22.2-22.3 Romains 11.35 Proverbes 9.12 Luc 17.10 Psaumes 16.2
8 Uovu wako waweza kumwumiza mtu kama wewe; Na haki yako yaweza kumfaa mwanadamu.
Psaumes 106.30 Job 42.8 Ecclésiaste 9.18 Josué 22.20 Genèse 12.2
9 Kwa sababu ya wingi wa jeuri wao hulia; Walilia msaada kwa sababu ya mkono wa wakuu.
Exode 2.23 Job 34.28 Psaumes 43.2 Néhémie 5.1-5.5 Job 40.9
10 Wala hapana asemaye, Yuko wapi Mungu Muumba wangu, Awapaye nyimbo wakati wa usiku;
Actes 16.25 Psaumes 42.8 Psaumes 149.5 Esaïe 51.13 Psaumes 77.6
11 Atufundishaye zaidi ya hayawani wa nchi, Na kutufanya wenye hekima kuliko ndege za angani?
Psaumes 94.12 Job 36.22 Genèse 1.26 Job 32.8 Genèse 2.7
12 Hulia huko, lakini hapana ajibuye, Kwa sababu ya kiburi cha watu waovu.
Proverbes 1.28 Jean 9.31 Psaumes 123.3-123.4 Psaumes 18.41 Esaïe 14.14-14.17
13 Hakika Mungu hatasikia ubatili, Wala Mwenyezi hatauangalia.
Proverbes 15.29 Esaïe 1.15 Jérémie 11.11 Jacques 4.3 Osée 7.14
14 Sembuse usemapo wewe ya kuwa humwangalii, Hiyo daawa i mbele yake, nawe wamngojea!
Job 9.11 Esaïe 50.10 Job 23.3 Job 23.8-23.10 Romains 8.33-8.34
15 Lakini sasa, kwa sababu yeye hakukujilia katika hasira zake, Wala hauangalii sana unyeti;
Psaumes 89.32 Hébreux 12.11-12.12 Job 13.15 Luc 1.20 Osée 11.8-11.9
16 Ndiposa Ayubu hufunua kinywa chake kwa ubatili; Huongeza maneno pasipo maarifa.
Job 38.2 Job 34.35-34.37 Job 3.1 Job 33.2 Job 33.8-33.12

Cette Bible est dans le domaine public.