Confiance dans l’intervention de Dieu
1 Bwana ndiye niliyemkimbilia. Mbona mnaiambia nafsi yangu, Kimbia kama ndege mlimani kwenu?
Psaumes 56.11 1 Samuel 23.14 Esaïe 26.3-26.4 Psaumes 31.14 1 Samuel 21.10-21.12
2 Maana, tazama, wasio haki wanaupinda uta, Wanaitia mishale yao katika upote, Ili kuwapiga gizani wanyofu wa moyo.
Jérémie 9.3 Psaumes 37.14 Psaumes 7.10 Psaumes 21.12 Psaumes 142.3
3 Kama misingi ikiharibika, Mwenye haki atafanya nini?
Psaumes 82.5 Actes 4.24-4.33 2 Timothée 2.19 2 Rois 22.12-22.14 Actes 4.5-4.12
4 Bwana yu katika hekalu lake takatifu. Bwana ambaye kiti chake kiko mbinguni, Macho yake yanaangalia; Kope zake zinawajaribu wanadamu.
Psaumes 18.6 Psaumes 103.19 Habakuk 2.20 Matthieu 5.34 Esaïe 66.1
5 Bwana humjaribu mwenye haki; Bali nafsi yake humchukia asiye haki, Na mwenye kupenda udhalimu.
Jacques 1.12 Genèse 22.1 Jérémie 12.8 Psaumes 139.23-139.24 1 Pierre 4.12
6 Awanyeshee wasio haki mitego, Moto na kiberiti na upepo wa hari, Na viwe fungu la kikombe chao.
Ezéchiel 38.22 Genèse 19.24 Psaumes 75.8 Job 18.15 1 Samuel 9.23
7 Kwa kuwa Bwana ndiye mwenye haki, Apenda matendo ya haki, Wanyofu wa moyo watamwona uso wake.
Psaumes 45.7 Psaumes 17.15 Psaumes 33.5 Apocalypse 22.4 Psaumes 42.5