Souffrance des exilés
1 Kando ya mito ya Babeli ndiko tulikoketi, Tukalia tulipoikumbuka Sayuni.Ezéchiel 1.1 Esaïe 66.10 Psaumes 102.9-102.14 Apocalypse 11.3 Lamentations 2.10-2.11
2 Katika miti iliyo katikati yake Tulivitundika vinubi vyetu.
Ezéchiel 26.13 Esaïe 24.8 Apocalypse 18.22 Psaumes 33.2 Psaumes 81.2
3 Maana huko waliotuchukua mateka Walitaka tuwaimbie; Na waliotuonea walitaka furaha; Tuimbieni baadhi ya nyimbo za Sayuni.
Psaumes 65.1 Esaïe 35.10 Psaumes 123.3-123.4 Lamentations 2.15-2.16 Psaumes 80.6
4 Tuuimbeje wimbo wa Bwana Katika nchi ya ugeni?
Amos 8.3 Osée 9.4 Esaïe 49.21 Lamentations 5.14-5.15 Esaïe 22.12
5 Ee Yerusalemu, nikikusahau wewe, Mkono wangu wa kuume na usahau.
Psaumes 122.5-122.9 Zacharie 11.17 Psaumes 84.1-84.2 Esaïe 62.6-62.7 Néhémie 1.2-1.4
6 Ulimi wangu na ugandamane Na kaakaa la kinywa changu, nisipokukumbuka. Nisipoikuza Yerusalemu Zaidi ya furaha yangu iliyo kuu.
Ezéchiel 3.26 Psaumes 22.15 Psaumes 84.10 1 Thessaloniciens 3.7-3.9 Actes 20.24
7 Ee Bwana, uwakumbuke wana wa Edomu, Siku ya Yerusalemu. Waliosema, Bomoeni! Bomoeni hata misingini!
Ezéchiel 25.12-25.14 Abdias 1.10-1.14 Jérémie 49.7-49.22 Lamentations 4.21-4.22 Osée 7.2
8 Ee binti Babeli, uliye karibu na kuangamia, Heri atakayekupatiliza, ulivyotupatiliza sisi.
Apocalypse 18.6 Esaïe 13.1-13.22 Psaumes 149.6-149.9 Esaïe 21.1 Zacharie 2.7
9 Heri yeye atakayewakamata wadogo wako, Na kuwaseta wao juu ya mwamba.
Esaïe 13.16 Osée 13.16 2 Rois 8.12 Nahum 3.10 Osée 10.14