1 Kando ya mito ya Babeli ndiko tulikoketi, Tukalia tulipoikumbuka Sayuni.
Ezéchiel 1.1 Lamentations 1.16 Ezéchiel 3.15 Jérémie 15.17 Daniel 10.2-10.3
2 Katika miti iliyo katikati yake Tulivitundika vinubi vyetu.
Esaïe 24.8 Ezéchiel 26.13 Psaumes 33.2 Psaumes 81.2 Amos 8.10
3 Maana huko waliotuchukua mateka Walitaka tuwaimbie; Na waliotuonea walitaka furaha; Tuimbieni baadhi ya nyimbo za Sayuni.
Jérémie 9.11 Psaumes 79.1 Michée 3.12 Apocalypse 14.1-14.3 Psaumes 65.1
4 Tuuimbeje wimbo wa Bwana Katika nchi ya ugeni?
Esaïe 49.21 Lamentations 5.14-5.15 Esaïe 22.12 Ecclésiaste 3.4 Amos 8.3
5 Ee Yerusalemu, nikikusahau wewe, Mkono wangu wa kuume na usahau.
Psaumes 84.10 Néhémie 2.2-2.3 Daniel 6.10-6.11 Jérémie 51.50 Psaumes 122.5-122.9
6 Ulimi wangu na ugandamane Na kaakaa la kinywa changu, nisipokukumbuka. Nisipoikuza Yerusalemu Zaidi ya furaha yangu iliyo kuu.
Ezéchiel 3.26 Psaumes 22.15 Matthieu 6.33 Job 29.10 Esaïe 41.17
7 Ee Bwana, uwakumbuke wana wa Edomu, Siku ya Yerusalemu. Waliosema, Bomoeni! Bomoeni hata misingini!
Abdias 1.10-1.14 Ezéchiel 25.12-25.14 Lamentations 4.21-4.22 Jérémie 49.7-49.22 Ezéchiel 35.2
8 Ee binti Babeli, uliye karibu na kuangamia, Heri atakayekupatiliza, ulivyotupatiliza sisi.
Apocalypse 18.6 Esaïe 13.1-13.22 Esaïe 44.28 Apocalypse 17.1-17.18 Psaumes 149.6-149.9
9 Heri yeye atakayewakamata wadogo wako, Na kuwaseta wao juu ya mwamba.
Esaïe 13.16 2 Rois 8.12 Osée 13.16 Nahum 3.10 Osée 10.14