Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 52
Bible en Swahili de l’est


1 Kwa nini kujisifia uovu, Ewe jabari? Wema wa Mungu upo sikuzote. Psaumes 94.4 1 Samuel 21.7 Psaumes 103.17 Psaumes 107.1 Genèse 6.4-6.5
2 Ulimi wako watunga madhara, Kama wembe mkali, Ewe mwenye hila Psaumes 57.4 Proverbes 18.21 Proverbes 12.18 Psaumes 59.7 Proverbes 30.14
3 Umependa mabaya kuliko mema, Na uongo kuliko kusema kweli. Michée 3.2 Jérémie 4.22 Jean 8.44 Apocalypse 22.15 Psaumes 62.4
4 Umependa maneno yote ya kupoteza watu, Ewe ulimi wenye hila. Jacques 3.6-3.9 Psaumes 120.3 1 Samuel 22.18-22.19
5 Lakini Mungu atakuharibu hata milele; Atakuondolea mbali; Atakunyakua hemani mwako; Atakung’oa katika nchi ya walio hai. Proverbes 2.22 Psaumes 27.13 Esaïe 38.11 Psaumes 140.9-140.11 Proverbes 12.19
6 Nao wenye haki wataona; Wataingiwa na hofu na kumcheka; Psaumes 40.3 Job 22.19 Psaumes 37.34 Malachie 1.5 Apocalypse 19.1-19.2
7 Kumbe! Huyu ndiye mtu yule, Asiyemfanya Mungu kuwa nguvu zake. Aliutumainia wingi wa mali zake, Na kujifanya hodari kwa madhara yake. Psaumes 73.7-73.11 1 Timothée 6.17 Psaumes 73.18-73.20 Psaumes 146.3-146.5 Job 31.24-31.25
8 Bali mimi ni kama mzeituni Umeao katika nyumba ya Mungu. Nazitumainia fadhili za Mungu milele na milele. Jérémie 11.16 Psaumes 92.12-92.14 Psaumes 13.5 Psaumes 1.3 Romains 11.24
9 Nitakushukuru milele kwa maana umetenda; Nitalingojea jina lako kwa kuwa ni jema; Mbele ya wacha Mungu wako. Psaumes 54.6 Psaumes 48.9-48.10 Psaumes 130.5-130.6 Psaumes 123.2-123.3 Proverbes 18.10

Cette Bible est dans le domaine public.