Prière et attitudes dans l’Église
1 Basi, kabla ya mambo yote, nataka dua, na sala, na maombezi, na shukrani, zifanyike kwa ajili ya watu wote;
2 Timothée 2.24 1 Timothée 2.4 Tite 3.2 Jacques 5.16 1 Thessaloniciens 3.12
2 kwa ajili ya wafalme na wote wenye mamlaka, tuishi maisha ya utulivu na amani, katika utauwa wote na ustahivu.
Esdras 6.10 Jérémie 29.7 1 Thessaloniciens 4.11 Romains 13.1-13.7 Proverbes 24.21
3 Hili ni zuri, nalo lakubalika mbele za Mungu Mwokozi wetu;
1 Timothée 1.1 Luc 1.47 1 Timothée 5.4 1 Pierre 2.20 Ephésiens 5.9-5.10
4 ambaye hutaka watu wote waokolewe, na kupata kujua yaliyo kweli.
Ezéchiel 18.32 Ezéchiel 18.23 2 Pierre 3.9 Tite 2.11 2 Timothée 2.25
5 Kwa sababu Mungu ni mmoja, na mpatanishi kati ya Mungu na wanadamu ni mmoja, Mwanadamu Kristo Yesu;
Galates 3.20 1 Corinthiens 8.6 Esaïe 44.6 Hébreux 7.25 Deutéronome 6.4
6 ambaye alijitoa mwenyewe kuwa ukombozi kwa ajili ya wote, utakaoshuhudiwa kwa majira yake.
Matthieu 20.28 1 Timothée 6.15 1 Corinthiens 1.6 Tite 1.3 Galates 4.4
7 Nami kwa ajili ya huo naliwekwa niwe mhubiri na mtume, (nasema kweli, sisemi uongo), mwalimu wa Mataifa katika imani na kweli.
2 Timothée 1.11 Actes 9.15 Ephésiens 3.7-3.8 Romains 9.1 Psaumes 111.7
8 Basi, nataka wanaume wasalishe kila mahali, huku wakiinua mikono iliyotakata pasipo hasira wala majadiliano.
Psaumes 134.2 Psaumes 63.4 Esaïe 1.15 Jérémie 7.9-7.10 Jean 4.21
9 Vivyo hivyo wanawake na wajipambe kwa mavazi ya kujisitiri, pamoja na adabu nzuri, na moyo wa kiasi; si kwa kusuka nywele, wala kwa dhahabu na lulu, wala kwa nguo za thamani;
Proverbes 31.22 Esaïe 3.16 Jérémie 2.32 1 Pierre 3.3-3.5 Jérémie 4.30
10 bali kwa matendo mema, kama iwapasavyo wanawake wanaoukiri uchaji wa Mungu.
Actes 9.36 Proverbes 31.31 Apocalypse 2.19 1 Pierre 3.3-3.5 Ephésiens 2.10
11 Mwanamke na ajifunze katika utulivu, akitii kwa kila namna.
1 Corinthiens 14.34-14.35 Genèse 3.16 1 Pierre 3.5-3.6 Esther 1.20 Colossiens 3.18
12 Simpi mwanamke ruhusa ya kufundisha, wala kumtawala mwanamume, bali awe katika utulivu.1 Corinthiens 14.34
13 Kwa maana Adamu ndiye aliyeumbwa kwanza, na Hawa baadaye.
Genèse 2.18 1 Corinthiens 11.8-11.9 Genèse 2.22 Genèse 2.7 Genèse 1.27
14 Wala Adamu hakudanganywa, ila mwanamke alidanganywa kabisa akaingia katika hali ya kukosa.
Genèse 3.6 2 Corinthiens 11.3 Genèse 3.12-3.13
15 Walakini ataokolewa kwa uzazi wake, kama wakidumu katika imani na upendo na utakaso, pamoja na moyo wa kiasi.
Tite 2.12 1 Pierre 4.7 1 Timothée 2.9 1 Timothée 1.5 Genèse 3.15-3.16