1 Heri aliyesamehewa dhambi, Na kusitiriwa makosa yake.
Romains 4.6-4.8 Psaumes 85.2 Actes 13.38-13.39 Esaïe 44.22 Michée 7.18-7.19
2 Heri Bwana asiyemhesabia upotovu, Ambaye rohoni mwake hamna hila.
Jean 1.47 1 Pierre 2.1-2.2 2 Corinthiens 5.19-5.21 Lévitique 17.4 Romains 5.13
3 Niliponyamaza mifupa yangu ilichakaa Kwa kuugua kwangu mchana kutwa.
Psaumes 38.8 Psaumes 22.1 Osée 7.14 2 Samuel 21.12-21.14 Psaumes 6.2
4 Kwa maana mchana na usiku Mkono wako ulinilemea. Jasho langu likakauka hata nikawa Kama nchi kavu wakati wa kaskazi.
Job 33.7 1 Samuel 5.11 Psaumes 22.15 Psaumes 102.3-102.4 Job 30.30
5 Nalikujulisha dhambi yangu, Wala sikuuficha upotovu wangu. Nalisema, Nitayakiri maasi yangu kwa Bwana, Nawe ukanisamehe upotovu wa dhambi yangu.
Esaïe 65.24 2 Samuel 12.13 Proverbes 28.13 Psaumes 38.18 Osée 6.1
6 Kwa hiyo kila mtu mtauwa Akuombe wakati unapopatikana. Hakika maji makuu yafurikapo, Hayatamfikia yeye.
Esaïe 55.6 Esaïe 43.2 Psaumes 42.7 Psaumes 4.3 Jean 7.34
7 Ndiwe sitara yangu, utanihifadhi na mateso, Utanizungusha nyimbo za wokovu.
Psaumes 9.9 Psaumes 119.114 Psaumes 31.20 Juges 5.1 Psaumes 27.5
8 Nitakufundisha na kukuonyesha njia utakayoiendea; Nitakushauri, jicho langu likikutazama.
Matthieu 11.29 Proverbes 3.5-3.6 Psaumes 33.18 Esaïe 49.10 Proverbes 3.1
9 Msiwe kama farasi wala nyumbu, Walio hawana akili. Kwa matandiko ya lijamu na hatamu Sharti kuwazuia hao, au hawatakukaribia.
Proverbes 26.3 Jacques 4.7-4.10 Job 35.11 Jacques 3.3 Jérémie 4.22
10 Naye mtu mwovu ana mapigo mengi, Bali amtumainiye Bwana fadhili zitamzunguka.
Proverbes 16.20 Proverbes 13.21 Psaumes 84.12 Psaumes 34.8 Psaumes 16.4
11 Mfurahieni Bwana; Shangilieni, enyi wenye haki Pigeni vigelegele vya furaha; Ninyi nyote mlio wanyofu wa moyo.
Psaumes 64.10 Psaumes 97.12 Psaumes 68.3 Philippiens 4.4 Psaumes 33.1