Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 56
Bible en Swahili de l’est


Confiance dans la détresse

1 Mungu, unirehemu, maana yuko atakaye kunimeza, Mchana kutwa ananionea akileta vita.
Psaumes 27.2 Psaumes 69.13-69.16 Psaumes 57.1-57.3 Psaumes 16.1 Lamentations 2.5
2 Adui zangu wanataka kunimeza mchana kutwa, Maana waletao vita juu yangu kwa kiburi ni wengi.
Daniel 5.18 Esaïe 57.15 Michée 6.6 Psaumes 92.8 Apocalypse 16.14
3 Siku ya hofu yangu nitakutumaini Wewe;
Psaumes 55.4-55.5 Psaumes 34.4 1 Samuel 30.6 1 Samuel 21.12 2 Corinthiens 7.5-7.6
4 Kwa msaada wa MUNGU nitalisifu neno lake. Nimemtumaini Mungu, sitaogopa; Mwenye mwili atanitenda nini?
Psaumes 118.6 Hébreux 13.6 Psaumes 56.10-56.11 Psaumes 119.160 Psaumes 27.1
5 Mchana kutwa wanapotosha maneno yangu, Mawazo yao yote ni juu yangu kunitakia mabaya.
2 Pierre 3.16 Luc 22.3-22.6 Luc 11.54 Jean 2.19 1 Samuel 18.21
6 Hukutanika, hujificha, huziangalia nyayo zangu, Kwa kuwa wameniotea nafsi yangu.
Psaumes 59.3 Psaumes 71.10 Psaumes 140.2 Psaumes 10.8-10.10 Psaumes 57.6
7 Je! Wataokoka kwa uovu wao? Ee Mungu, uwaangamize kwa hasira yako.
Psaumes 55.23 Psaumes 36.12 Ecclésiaste 8.8 Jérémie 10.25 Esaïe 28.15
8 Umehesabu kutanga-tanga kwangu; Uyatie machozi yangu katika chupa yako; (Je! Hayamo katika kitabu chako?)
Psaumes 39.12 2 Rois 20.5 Malachie 3.16 Matthieu 10.30 Psaumes 139.16
9 Ndipo adui zangu watarudi nyuma siku ile niitapo. Neno hili najua kuwa MUNGU yu upande wangu;
Romains 8.31 Psaumes 118.6 Psaumes 102.2 Psaumes 118.11-118.13 Psaumes 46.11
10 Kwa msaada wa MUNGU nitalisifu neno lake. Kwa msaada wa Bwana nitalisifu neno lake.
Psaumes 56.4 Genèse 32.11 Hébreux 6.18 2 Pierre 1.4 Matthieu 24.35
11 Nimemtumaini Mungu, sitaogopa; Mwanadamu atanitenda nini?
Esaïe 51.12-51.13 Psaumes 112.7-112.8 Esaïe 51.7-51.8 Psaumes 27.1
12 Ee Mungu, nadhiri zako zi juu yangu; Nitakutolea dhabihu za kushukuru.
Psaumes 50.14 Psaumes 9.1-9.3 Nombres 30.2-30.16 Psaumes 59.16-59.17 Psaumes 21.13
13 Maana umeniponya nafsi yangu na mauti; Je! Hukuizuia miguu yangu isianguke? Ili nienende mbele za Mungu Katika nuru ya walio hai.
Psaumes 116.8-116.9 Job 33.30 Apocalypse 21.23-21.24 Esaïe 38.3 Genèse 17.1

Cette Bible est dans le domaine public.