Dieu, seul auteur du salut
1 Ole wao watelemkao kwenda Misri wapate msaada, na kutegemea farasi; watumainio magari kwa kuwa ni mengi, na wapanda farasi kwa kuwa ni hodari sana; lakini hawamwangalii Mtakatifu wa Israeli, wala hawamtafuti Bwana!
Psaumes 20.7 Esaïe 36.6 Deutéronome 17.16 Daniel 9.13 Esaïe 30.16
2 Lakini yeye naye ana akili, naye ataleta uovu, wala hatayatangua maneno yake; bali ataondoka juu ya nyumba yao watendao mabaya, na juu ya msaada wa hao watendao maovu.
Nombres 23.19 Esaïe 45.7 Psaumes 12.5-12.6 Zacharie 1.6 Sophonie 3.8
3 Basi Wamisri ni wanadamu wala si Mungu, na farasi zao ni nyama wala si roho; na Bwana atakaponyosha mkono wake, yeye asaidiaye atajikwaa, na yeye asaidiwaye ataanguka, nao wote pamoja watakoma.
Esaïe 9.17 Ezéchiel 28.9 Ezéchiel 20.33-20.34 Jérémie 15.6 Deutéronome 32.30-32.31
4 Maana Bwana aniambia hivi, Kama vile ilivyo simba angurumapo na mwana-simba juu ya mawindo yake, wachungaji wengi wakiitwa ili kumpiga, lakini hatiwi hofu na sauti zao, wala kufanya woga kwa sababu ya mshindo wao; ndivyo Bwana wa majeshi atakavyoshuka ili kufanya vita juu ya mlima Sayuni, na juu ya kilima chake.
Amos 3.8 Esaïe 42.13 Osée 11.10 Zacharie 12.8 Nombres 24.8-24.9
5 Kama ndege warukao, Bwana wa majeshi ataulinda Yerusalemu; ataulinda na kuuokoa, atapita juu yake na kuuhifadhi.
Deutéronome 32.11 Psaumes 91.4 Esaïe 38.6 Esaïe 37.35 Psaumes 37.40
6 Mwelekeeni yeye mliyemwasi sana, enyi wana wa Israeli.
Jérémie 3.14 Esaïe 55.7 Jérémie 3.10 Jérémie 3.22 Joël 2.12-2.13
7 Maana katika siku hiyo kila mtu atatupa sanamu zake za fedha, na sanamu zake za dhahabu, ambazo mikono yenu imezifanya, zikawa dhambi kwenu.Esaïe 2.20 Esaïe 30.22 Osée 8.11 Osée 14.8 1 Rois 12.28-12.30
8 Ndipo huyo Mwashuri ataanguka kwa upanga ambao si wa mtu; na upanga usio upanga wa mtu utamla; naye ataukimbia upanga, na vijana wake watatoa kodi.
Esaïe 14.25 Genèse 49.15 2 Rois 19.34-19.37 Esaïe 37.35-37.38 Esaïe 29.5
9 Na mwamba wake utatoweka kwa sababu ya hofu, nao wakuu wake wataionea bendera hofu kuu, asema Bwana, ambaye moto wake u katika Sayuni, na tanuru yake katika Yerusalemu.
Esaïe 29.6 Esaïe 10.17 Malachie 4.1 Esaïe 18.3 Zacharie 2.5