1 Roho ya Bwana MUNGU i juu yangu; kwa sababu Bwana amenitia mafuta niwahubiri wanyenyekevu habari njema; amenituma ili kuwaganga waliovunjika moyo, kuwatangazia mateka uhuru wao, na hao waliofungwa habari za kufunguliwa kwao.
Luc 4.18-4.19 Luc 7.22 Esaïe 42.7 Matthieu 11.5 Psaumes 147.3
2 Kutangaza mwaka wa Bwana uliokubaliwa, na siku ya kisasi cha Mungu wetu; kuwafariji wote waliao;
Matthieu 5.4 Esaïe 34.8 Jérémie 31.13 Esaïe 57.18 Luc 4.19
3 kuwaagizia hao waliao katika Sayuni, wapewe taji ya maua badala ya majivu, mafuta ya furaha badala ya maombolezo, vazi la sifa badala ya roho nzito; wapate kuitwa miti ya haki, iliyopandwa na Bwana, ili atukuzwe.
Jérémie 17.7-17.8 Esaïe 61.10 Jean 16.20 Psaumes 45.7 Psaumes 30.11
4 Nao watajenga mahali pa kale palipoharibiwa, watapainua mahali palipokuwa ukiwa zamani, watatengeneza miji iliyoharibiwa, mahali palipoachwa kizazi baada ya kizazi.
Esaïe 58.12 Esaïe 49.6-49.8 Ezéchiel 36.23-36.26 Ezéchiel 36.33-36.36 Amos 9.14-9.15
5 Na wageni watasimama na kulisha makundi yenu, na watu wa kabila nyingine watakuwa wakulima wenu, na watunzaji wa mizabibu yenu.
Esaïe 14.1-14.2 Esaïe 60.10-60.14 Ephésiens 2.12-2.20
6 Bali ninyi mtaitwa makuhani wa Bwana; watu watawaiteni wahudumu wa Mungu wetu; mtakula utajiri wa mataifa, na kujisifia utukufu wao.
Exode 19.6 1 Pierre 2.9 1 Pierre 2.5 Esaïe 60.5-60.7 Esaïe 66.21
7 Badala ya aibu yenu mtapata maradufu, na badala ya fedheha wataifurahia sehemu yao; basi katika nchi yao watamiliki maradufu; furaha yao itakuwa ya milele.
Esaïe 40.2 Zacharie 9.12 Psaumes 16.11 Esaïe 51.11 Matthieu 25.46
8 Maana mimi, Bwana, naipenda hukumu ya haki, nauchukia wivi na uovu; nami nitawalipa malipo katika kweli, nitaagana nao agano la milele.
Esaïe 55.3 Psaumes 11.7 Jérémie 32.40 Genèse 17.7 Jérémie 9.24
9 Na kizazi chao kitajulikana katika mataifa, na uzao wao katika kabila za watu; wote wawaonao watakiri ya kuwa wao ni kizazi kilichobarikiwa na Bwana.
Esaïe 44.3 Actes 3.26 Esaïe 65.23 Psaumes 115.14 Zacharie 8.13
10 Nitafurahi sana katika Bwana, nafsi yangu itashangilia katika Mungu wangu; maana amenivika mavazi ya wokovu, amenifunika vazi la haki, kama bwana arusi ajipambavyo kwa kilemba cha maua, na kama bibi arusi ajipambavyo kwa vyombo vya dhahabu.
Apocalypse 19.7-19.8 Esaïe 49.18 Apocalypse 21.2 Psaumes 132.9 Psaumes 132.16
11 Maana kama nchi itoavyo machipuko yake, na kama bustani ioteshavyo vitu vilivyopandwa ndani yake; ndivyo Bwana MUNGU atakavyootesha haki na sifa mbele ya mataifa yote.
Psaumes 85.11 Esaïe 60.18 Esaïe 62.7 Psaumes 72.3 Esaïe 62.1