Louange universelle de la création
1 Haleluya. Msifuni Bwana kutoka mbinguni; Msifuni katika mahali palipo juu.
Psaumes 69.34 Apocalypse 19.1-19.6 Psaumes 89.5 Luc 2.13-2.14 Esaïe 49.13
2 Msifuni, enyi malaika wake wote; Msifuni, majeshi yake yote.
Psaumes 103.20-103.21 Esaïe 6.2-6.4 Job 38.7 Genèse 2.1 Ezéchiel 3.12
3 Msifuni, jua na mwezi; Msifuni, nyota zote zenye mwanga.
Psaumes 19.1-19.6 Jérémie 33.20 Psaumes 89.36-89.37 Deutéronome 4.19 Genèse 1.14-1.16
4 Msifuni, enyi mbingu za mbingu, Nanyi maji mlioko juu ya mbingu.
Genèse 1.7 1 Rois 8.27 Psaumes 68.33 Genèse 7.11 Psaumes 113.6
5 Na vilisifu jina la Bwana, Kwa maana aliamuru, vikaumbwa.
Psaumes 33.6-33.9 Genèse 1.6 Apocalypse 4.11 Amos 9.6 Psaumes 95.5
6 Amevithibitisha hata milele na milele, Ametoa amri wala haitapita.
Jérémie 33.25 Jérémie 31.35-31.36 Psaumes 89.37 Job 38.33 Psaumes 119.90-119.91
7 Msifuni Bwana kutoka nchi, Enyi nyangumi na vilindi vyote.
Genèse 1.21 Psaumes 74.13-74.14 Psaumes 104.25-104.26 Job 41.1-41.34 Esaïe 51.9-51.10
8 Moto na mvua ya mawe, theluji na mvuke, Upepo wa dhoruba ulitendao neno lake.
Psaumes 147.15-147.18 Psaumes 18.12 Lévitique 10.2 Job 37.2-37.6 Nombres 16.35
9 Milima na vilima vyote, Miti yenye matunda na mierezi yote.
Esaïe 44.23 Esaïe 49.13 Psaumes 97.4-97.5 Psaumes 96.11-96.13 Esaïe 42.11
10 Hayawani, na wanyama wafugwao, Vitambaavyo, na ndege wenye mbawa.
Psaumes 50.10-50.11 Genèse 1.20-1.25 Psaumes 150.6 Ezéchiel 17.23 Psaumes 103.22
11 Wafalme wa dunia, na watu wote, Wakuu, na makadhi wote wa dunia.
Psaumes 102.15 Psaumes 68.31-68.32 Psaumes 138.4-138.5 Apocalypse 21.24 Psaumes 22.27-22.29
12 Vijana waume, na wanawali, Wazee, na watoto;
Psaumes 8.2 Luc 19.37 Psaumes 68.25 Matthieu 21.15-21.16 Zacharie 9.17
13 Na walisifu jina la Bwana, Maana jina lake peke yake limetukuka; Adhama yake i juu ya nchi na mbingu.
Psaumes 113.4 Psaumes 8.1 Esaïe 12.4 Ephésiens 4.10 Esaïe 33.5
14 Naye amewainulia watu wake pembe, Sifa za watauwa wake wote; Wana wa Israeli, watu walio karibu naye. Haleluya.
1 Samuel 2.1 Psaumes 75.10 Ephésiens 2.17 Deutéronome 4.7 Apocalypse 5.8-5.14