Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 86.12
Bible en Swahili de l’est


Appel à la grâce de Dieu

1 Ee Bwana, utege sikio lako unijibu, Maana mimi ni maskini na mhitaji
Psaumes 31.2 Psaumes 40.17 Daniel 9.18 Matthieu 5.3 Esaïe 37.17
2 Unihifadhi nafsi yangu, Maana mimi ni mcha Mungu. Wewe uliye Mungu wangu, Umwokoe mtumishi wako anayekutumaini.
Ephésiens 1.12-1.13 Psaumes 4.3 Psaumes 13.5 Deutéronome 7.7-7.8 Psaumes 119.124-119.125
3 Wewe, Bwana, unifadhili, Maana nakulilia Wewe mchana kutwa.
Psaumes 57.1 Psaumes 88.9 Ephésiens 6.18 Psaumes 25.5 Psaumes 56.1
4 Uifurahishe nafsi ya mtumishi wako, Maana nafsi yangu nakuinulia Wewe, Bwana.
Psaumes 25.1 Psaumes 143.8 Psaumes 51.12 Esaïe 66.13-66.14 Esaïe 61.3
5 Kwa maana Wewe, Bwana, U mwema, Umekuwa tayari kusamehe, Na mwingi wa fadhili, Kwa watu wote wakuitao.
Joël 2.13 Psaumes 103.8 Exode 34.6 Néhémie 9.17 Psaumes 145.8-145.9
6 Ee Bwana, uyasikie maombi yangu; Uisikilize sauti ya dua zangu.
Psaumes 5.1-5.2 Psaumes 130.2 Psaumes 55.1 Psaumes 17.1
7 Siku ya mateso yangu nitakuita, Kwa maana utaniitikia.
Psaumes 50.15 Psaumes 17.6 Psaumes 34.4-34.6 Jonas 2.2 Lamentations 3.55-3.57
8 Katikati ya miungu hakuna kama Wewe, Bwana, Wala matendo mfano wa matendo yako.
Psaumes 89.6 Deutéronome 3.24 Exode 15.11 Jérémie 10.6-10.7 Jérémie 10.16
9 Mataifa yote uliowafanya watakuja; Watakusujudia Wewe, Bwana, Watalitukuza jina lako;
Psaumes 66.4 Apocalypse 15.4 Esaïe 66.23 Romains 15.9 Esaïe 43.7
10 Kwa kuwa ndiwe uliye mkuu, Wewe ndiwe mfanya miujiza, Ndiwe Mungu peke yako.
Psaumes 72.18 Marc 12.29 Esaïe 37.16 1 Corinthiens 8.4 Deutéronome 32.39
11 Ee Bwana, unifundishe njia yako; Nitakwenda katika kweli yako; Moyo wangu na ufurahi kulicha jina lako;
Jérémie 32.38-32.39 1 Corinthiens 10.21 Psaumes 5.8 Job 34.32 Psaumes 26.3
12 Nitakusifu Wewe, Bwana, Mungu wangu, Kwa moyo wangu wote, Nitalitukuza jina lako milele.
Deutéronome 6.5 1 Corinthiens 10.31 Romains 15.6 Apocalypse 5.9-5.13 1 Corinthiens 6.20
13 Maana fadhili zako kwangu ni nyingi sana; Umeiopoa nafsi yangu na kuzimu.
Luc 1.58 Psaumes 103.8-103.12 1 Thessaloniciens 1.10 Psaumes 88.6 Psaumes 30.3
14 Ee Mungu, wenye kiburi wamenishambulia; Mkutano wa wakatili wamenitafuta roho. Wala hawakukuweka Wewe Mbele ya macho yao.
Psaumes 54.3 Psaumes 140.5 Psaumes 119.51 Psaumes 10.11 Psaumes 119.85
15 Lakini Wewe, Bwana, U Mungu wa rehema na neema, Mvumilivu, mwingi wa fadhili na kweli.
Psaumes 103.8 Néhémie 9.17 Psaumes 111.4 Psaumes 86.5 Joël 2.13
16 Unielekee na kunifadhili mimi; Mpe mtumishi wako nguvu zako, Umwokoe mwana wa mjakazi wako.
Psaumes 25.16 Psaumes 116.16 Psaumes 90.13 Psaumes 119.132 Colossiens 1.11
17 Unifanyie ishara ya wema, Wanichukiao waione na kuaibishwa. Kwa kuwa Wewe, Bwana, Umenisaidia na kunifariji.
Psaumes 41.10-41.11 1 Corinthiens 5.5 Psaumes 40.1 Psaumes 71.20-71.21 Juges 6.17

Cette Bible est dans le domaine public.