1 Paulo, mtumwa wa Mungu, na mtume wa Yesu Kristo; kwa ajili ya imani ya wateule wa Mungu, na ujuzi wa kweli ile iletayo utauwa;
Romains 1.1 1 Timothée 6.3 Tite 2.11-2.12 2 Timothée 2.23 2 Pierre 1.3
2 katika tumaini la uzima wa milele, ambao Mungu asiyeweza kusema uongo aliuahidi tangu milele;
2 Timothée 1.1 Tite 3.7 2 Timothée 1.9 Tite 2.13 Hébreux 6.17-6.18
3 akalifunua neno lake kwa majira yake katika ule ujumbe niliowekewa amana mimi kwa amri ya Mwokozi wetu Mungu;
1 Timothée 1.11 1 Timothée 1.1 Tite 2.10 Tite 3.4-3.6 Apocalypse 14.16
4 kwa Tito, mwanangu hasa katika imani tuishirikiyo. Neema na iwe kwako na amani zitokazo kwa Mungu Baba na kwa Kristo Yesu Mwokozi wetu.
Jude 1.3 2 Timothée 1.2 2 Pierre 1.1 2 Corinthiens 2.13 Galates 2.3
5 Kwa sababu hii nalikuacha Krete, ili uyatengeneze yaliyopunguka, na kuweka wazee katika kila mji kama vile nilivyokuamuru;
Actes 14.23 1 Timothée 1.3 Actes 27.7 2 Timothée 2.2 Ecclésiaste 12.9
6 ikiwa mtu hakushitakiwa neno, naye ni mume wa mke mmoja, ana watoto waaminio, wasioshitakiwa kuwa ni wafisadi wala wasiotii.
1 Timothée 3.12 1 Timothée 3.2-3.7 Tite 1.6-1.8 Ezéchiel 44.22 Tite 1.10
7 Maana imempasa askofu awe mtu asiyeshitakiwa neno ,kwa kuwa ni wakili wa MUNGU;asiwe mtu wa kujipendeza nafsi yake,asiwe mwepesi wa hasira,asiwe mlevi wala mgomvi,asiwe mpenda mapato ya aibu.
2 Pierre 2.10 1 Pierre 5.2 Luc 12.42 Ephésiens 5.18 Lévitique 10.9
8 bali awe mkaribishaji, mpenda wema, mwenye kiasi, mwenye haki, mtakatifu, mwenye kudhibiti nafsi yake;
1 Timothée 3.2 1 Thessaloniciens 2.10 2 Timothée 3.3 1 Timothée 6.11 2 Corinthiens 6.4-6.8
9 akilishika lile neno la imani vile vile kama alivyofundishwa, apate kuweza kuwaonya watu kwa mafundisho yenye uzima, na kuwashinda wenye kupinga.
1 Timothée 1.10 2 Thessaloniciens 2.15 1 Timothée 6.3 2 Timothée 1.13 Tite 2.1
10 Kwa maana kuna wengi wasiotii, wenye maneno yasiyo na maana, wadanganyaji, na hasa wale wa tohara, ambao yapasa wazibwe vinywa vyao.
1 Timothée 1.6 Actes 11.2 Apocalypse 2.6 1 Jean 2.18 2 Timothée 4.4
11 Hao wanapindua watu wa nyumba nzima, wakifundisha yasiyowapasa kwa ajili ya mapato ya aibu.2 Timothée 3.6 1 Timothée 6.5 Esaïe 56.10-56.11 Jérémie 8.10 Psaumes 63.11
12 Mtu wa kwao, nabii wao wenyewe, amesema, Wakrete ni waongo siku zote, hayawani wabaya, walafi wavivu.
Actes 17.28 1 Timothée 4.2 Actes 2.11 Romains 16.18 2 Pierre 2.15
13 Ushuhuda huo ni kweli. Kwa sababu hiyo uwakemee kwa ukali, ili wapate kuwa wazima katika imani;
Tite 2.2 2 Corinthiens 13.10 Tite 2.15 1 Timothée 5.20 2 Timothée 4.2
14 wasisikilize hadithi za Kiyahudi, wala maagizo ya watu wajiepushao na yaliyo kweli.
Colossiens 2.22 2 Timothée 4.4 Hébreux 12.25 Matthieu 15.9 2 Pierre 2.22
15 Vitu vyote ni safi kwa hao walio safi; lakini hakuna kilicho safi kwao walio wanajisi, wasioamini; bali akili zao zimekuwa najisi, na nia zao pia.
Romains 14.20 Romains 14.14 Romains 14.23 1 Corinthiens 10.23 1 Timothée 4.3-4.4
16 Wanakiri ya kwamba wanamjua Mungu, bali kwa matendo yao wanamkana; ni wenye machukizo, waasi, wala kwa kila tendo jema hawafai.
1 Jean 2.4 Esaïe 29.13 Ezéchiel 33.31 2 Timothée 3.5-3.8 Jude 1.4