Confiance du psalmiste trahie par un ami
1 Ee Mungu, uisikilize sala yangu, Wala usijifiche nikuombapo rehema.
Psaumes 61.1 1 Pierre 3.12 Psaumes 17.1 Psaumes 54.1-54.2 Psaumes 86.6
2 Unisikilize na kunijibu, Nimetanga-tanga nikilalama na kuugua.
Esaïe 38.14 Esaïe 59.11 Psaumes 64.1 Psaumes 38.6 Psaumes 102.9-102.10
3 Kwa sababu ya sauti ya adui, Kwa sababu ya dhuluma yake yule mwovu. Kwa maana wananitupia uovu, Na kwa ghadhabu wananiudhi.
2 Samuel 16.7-16.8 2 Samuel 19.19 Psaumes 12.5 Matthieu 26.59 Psaumes 35.11
4 Moyo wangu unaumia ndani yangu, Na hofu za mauti zimeniangukia.
Psaumes 116.3 Psaumes 18.4-18.5 Psaumes 88.3 Jean 12.27 Psaumes 102.3-102.5
5 Hofu na tetemeko limenijia, Na hofu kubwa imenifunikiza.
Psaumes 119.120 Job 21.6 Psaumes 88.15-88.16 Psaumes 42.6 Luc 22.44
6 Nikasema, Ningekuwa na mbawa kama njiwa, Ningerukia mbali na kustarehe.
Apocalypse 12.14 Psaumes 11.1 Psaumes 139.9
7 Ningekwenda zangu mbali, Ningetua jangwani.Jérémie 9.2 Jérémie 37.12 1 Samuel 27.1 Proverbes 6.4-6.5 2 Samuel 15.14
8 Ningefanya haraka kuzikimbia Dhoruba na tufani.
Esaïe 4.6 Matthieu 7.25-7.27 Esaïe 17.12-17.13 Psaumes 18.4
9 Ee Bwana, uwaangamize, uzichafue ndimi zao, Maana nimeona dhuluma na fitina katika mji.
Jérémie 6.7 2 Samuel 15.31 2 Samuel 17.1-17.14 Genèse 11.7-11.9 Matthieu 23.37-23.38
10 Mchana na usiku huzunguka kutani mwake; Uovu na taabu zimo ndani yake;
Psaumes 59.14-59.15 2 Samuel 16.21-16.22 Psaumes 59.6 Ezéchiel 9.4 Michée 2.1-2.2
11 Tamaa mbaya zimo ndani yake; Dhuluma na hila haziondoki mitaani mwake.
Jérémie 5.26-5.27 Psaumes 10.7 Ezéchiel 22.1-22.12 Jérémie 9.3-9.5 Psaumes 109.2-109.3
12 Kwa maana aliyetukana si adui; Kama ndivyo, ningevumilia. Aliyejitukuza juu yangu siye anichukiaye; Kama ndivyo, ningejificha asinione.
Psaumes 41.9 Matthieu 26.21-26.23 Jean 13.18 Psaumes 35.26 Jean 18.2-18.3
13 Bali ni wewe, mtu mwenzangu, Rafiki yangu, niliyejuana nawe sana.
2 Samuel 15.12 Psaumes 41.9 Michée 7.5 2 Samuel 16.23 Jérémie 9.4
14 Tulipeana shauri tamu; na kutembea Nyumbani mwa Mungu pamoja na mkutano.
Psaumes 42.4 Esaïe 2.3 Ezéchiel 33.31 Psaumes 122.1
15 Mauti na iwapate kwa ghafula, Na washuke kuzimu wangali hai, Maana uovu u makaoni mwao na katikati yao.
2 Samuel 18.9 Psaumes 59.13 Psaumes 109.6-109.20 Psaumes 9.17 2 Samuel 18.14
16 Nami nitamwita Mungu, Na Bwana ataniokoa;
Psaumes 50.15 Psaumes 109.4 Psaumes 73.28 Psaumes 91.15 Luc 6.11-6.12
17 Jioni, asubuhi, na adhuhuri nitalalama na kuugua, Naye ataisikia sauti yangu.
Actes 3.1 Ephésiens 6.18 Psaumes 141.2 1 Thessaloniciens 5.17 Actes 10.30
18 Ameiokoa nafsi yangu iwe salama, asinikaribie mtu, Maana walioshindana nami walikuwa wengi.
Psaumes 57.3 Psaumes 118.10-118.12 2 Rois 6.16 Psaumes 56.2 Actes 2.33-2.36
19 Mungu atasikia na kuwajibu; Ndiye Yeye akaaye tangu milele. Mageuzi ya mambo hayawapati hao, Kwa hiyo hawamchi Mungu.
Deutéronome 33.27 Sophonie 1.12 Apocalypse 6.10-6.11 Colossiens 1.17 Esaïe 36.20
20 Amenyosha mkono awadhuru waliopatana naye, Amelihalifu agano lake.
Psaumes 7.4 Psaumes 89.34 Actes 12.1 1 Samuel 24.10 Ezéchiel 17.16-17.19
21 Kinywa chake ni laini kuliko siagi, Bali moyo wake ni vita. Maneno yake ni mororo kuliko mafuta, Bali hayo ni panga wazi.
Psaumes 28.3 Proverbes 5.3-5.4 Psaumes 57.4 Proverbes 26.28 Psaumes 59.7
22 Umtwike Bwana mzigo wako naye atakutegemeza, Hatamwacha mwenye haki aondoshwe milele.
Psaumes 37.5 1 Pierre 5.7 Matthieu 6.25 Philippiens 4.6-4.7 Psaumes 37.24
23 Nawe, Ee Mungu, utawatelemsha, Walifikilie shimo la uharibifu; Watu wa damu na hila hawataishi nusu ya siku zao, Bali mimi nitakutumaini Wewe.
Job 15.32 Psaumes 5.6 Proverbes 10.27 Esaïe 38.17 Psaumes 73.18