1 Mpendwa wako amekwenda wapi, Wewe uliye mzuri katika wanawake? Mpendwa wako amegeukia upande upi, Ili tumtafute pamoja nawe?
Cantique 1.8 Cantique 5.9 Esaïe 2.5 Cantique 6.4 Cantique 5.6
2 Mpendwa wangu ameshukia bustani yake, Kwenye matuta ya rihani; Ili kulisha penye bustani, Ili kuchuma nyinyoro.
Cantique 5.13 Esaïe 57.1 Jean 14.3 Philippiens 1.21-1.23 Cantique 6.11
3 Mimi ni wake mpendwa wangu, naye ni wangu, Hulisha kundi lake penye nyinyoro.
Cantique 2.16 Cantique 7.10 Apocalypse 21.2-21.4 Hébreux 8.10
4 Mpenzi wangu, u mzuri kama Tirza, Mwenye kupendeza kama Yerusalemu, Wa kutisha kama wenye bendera.
Cantique 6.10 Psaumes 48.2 1 Rois 14.17 Psaumes 50.2 Cantique 4.7
5 Uyageuzie macho yako mbali nami, Kwa maana yamenitisha sana. Nywele zako ni kama kundi la mbuzi, Wakijilaza mbavuni pa Gileadi.
Cantique 4.1-4.3 Jérémie 15.1 Genèse 32.26-32.28 Exode 32.10 Matthieu 15.27-15.28
6 Meno yako kama kundi la kondoo, Wakipanda kutoka kuoshwa; Ambao kila mmoja amezaa mapacha, Wala hakuna aliyefiwa kati yao.
Cantique 4.2 Matthieu 25.30 Matthieu 21.19
7 Mashavu yako ni kama kipande cha komamanga, Nyuma ya barakoa yako.
Cantique 4.3
8 Wako malkia sitini, na masuria themanini, Na wanawali wasiohesabika;
Psaumes 45.14 Psaumes 45.9 1 Rois 11.1 Apocalypse 7.9 2 Chroniques 11.21
9 Hua wangu, mkamilifu wangu, ni mmoja tu, Mtoto wa pekee wa mamaye. Ndiye kipenzi chake aliyemzaa, Binti wakamwona wakamwita heri; Malkia na masuria nao wakamwona, Wakamsifu, wakisema,
Cantique 5.2 Cantique 2.14 Ephésiens 4.3-4.6 Deutéronome 4.6-4.7 Nombres 23.9
10 Ni nani huyu atazamaye kama alfajiri, Mzuri kama mwezi, safi kama jua, Wa kutisha kama wenye bendera?
Cantique 6.4 Job 31.26 2 Samuel 23.4 Esaïe 58.8 Matthieu 17.2
11 Nalishukia bustani ya milozi, Ili kuyatazama machipuko ya bondeni; Nione kama mzabibu umechanua, Kama mikomamanga imetoa maua.
Cantique 7.12 Luc 13.7 Genèse 2.9 Jean 15.16 Cantique 4.12-4.15
12 Kabla sijajua, roho yangu ilinileta Katikati ya magari ya wakuu wangu.
Luc 15.20 Osée 11.8-11.9 Jérémie 31.18-31.20
13 Rudi, rudi, Mshulami, Rudi, rudi, ili sisi tukutazame.
Genèse 32.2 Ephésiens 2.14-2.17 Cantique 2.14 Esaïe 8.6 Galates 5.17