Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Cantique 7.4
Bible en Swahili de l’est


Les filles de Jérusalem

1 Siti msharifu, jinsi zilivyo nzuri Hatua zako katika mitalawanda. Mapaja yako ya mviringo ni kama johari, Kazi ya mikono ya fundi mstadi;
Psaumes 45.13 Exode 28.15 Luc 15.22 Daniel 2.32 Exode 35.35

Le jeune homme

2 Kitovu chako ni kama bilauri iliyoviringana, Na isikose divai iliyochanganyika; Tumbo lako ni mfano wa chungu ya ngano, Iliyozungukwa na ugo wa nyinyoro;
Psaumes 45.16 Esaïe 46.3 Proverbes 3.8 Cantique 5.14 Jérémie 1.5
3 Maziwa yako mawili ni kama wana-paa wawili, Ambao ni mapacha ya paa;
Cantique 4.5 Cantique 6.6
4 Shingo yako ni kama huo mnara wa pembe; Macho yako kama viziwa vya Heshboni, Karibu na mlango wa Beth-rabi; Pua yako ni kama mnara wa Lebanoni, Unaoelekea Dameski;
Cantique 4.4 Psaumes 144.12 Cantique 1.10 Psaumes 45.8 Cantique 6.5
5 Kichwa chako juu yako ni kama Karmeli, Na nywele za kichwa chako kama urujuani, Mfalme amenaswa na mashungu yake.
Esaïe 35.2 Cantique 4.1 Psaumes 87.2 Genèse 32.26 Colossiens 1.18
6 Jinsi yalivyo mazuri, yalivyo matamu, Mapenzi katikati ya anasa!
Cantique 1.15-1.16 Cantique 4.10 Psaumes 45.11 Cantique 4.7 Sophonie 3.17
7 Kimo chako kimefanana na mtende, Na maziwa yako na vichala.
Cantique 4.5 Ephésiens 3.17 Ephésiens 4.13 Cantique 8.8 Psaumes 92.12
8 Nilisema, Nitapanda huo mtende, Na kuyashika makuti yake. Maziwa yako na yawe kama vichala vya mzabibu, Na harufu ya pumzi yako kama mapera;
Jean 14.21-14.23 2 Corinthiens 2.14 Cantique 1.3 Jérémie 32.41 Cantique 2.5
9 Na kinywa chako kama divai iliyo bora, Kwa mpendwa wangu inashuka taratibu, Ikitiririka midomoni mwao walalao.
Cantique 5.16 Hébreux 13.15 Esaïe 62.8-62.9 Cantique 5.2 Cantique 2.14
10 Mimi ni wake mpendwa wangu, Na shauku yake ni juu yangu.
Cantique 2.16 Psaumes 45.11 Cantique 6.3 Galates 2.20 1 Corinthiens 6.19-6.20
11 Njoo, mpendwa wangu, twende mashambani, Tufanye maskani katika vijiji.
Cantique 4.8 Cantique 1.4 Cantique 2.10-2.13
12 Twende mapema hata mashamba ya mizabibu, Tuone kama mzabihu umechanua, Na maua yake yamefunuka; Kama mikomamanga imetoa maua; Huko nitakupa pambaja zangu.
Cantique 6.11 Ephésiens 6.24 Cantique 2.13 Cantique 7.6 Psaumes 43.4
13 Mitunguja hutoa harufu yake; Juu ya milango yetu yako matunda mazuri, Mapya na ya kale, ya kila namna, Niliyokuwekea, mpendwa wangu.
Genèse 30.14 Matthieu 13.52 Cantique 4.16-5.1 Philippiens 1.11 1 Corinthiens 16.2

Cette Bible est dans le domaine public.