Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Osée 7
Bible en Swahili de l’est


Reproches contre les alliances politiques

1 Wakati nitakapo kumponya Israeli, ndipo yafunuliwapo maovu ya Efraimu, na ubaya wa Samaria; maana wanatenda uongo, na mwivi huvunja nyumba za watu, na kundi la wanyang’anyi hushambulia nje.
Osée 4.2 Osée 6.4 Luc 13.34 Osée 8.5 Amos 8.14
2 Wala hawafikiri mioyoni mwao ya kwamba naukumbuka uovu wao wote; sasa matendo yao wenyewe yamewazunguka pande zote; yako mbele za uso wangu.
Jérémie 2.19 Jérémie 14.10 Psaumes 90.8 Luc 12.2 Psaumes 9.16
3 Humfurahisha mfalme kwa uovu wao, na wakuu wao kwa uongo wao.
Romains 1.32 Michée 7.3 Jérémie 28.1-28.4 Osée 5.11 Jérémie 9.2
4 Hao wote ni wazinzi; wamekuwa kama tanuu iliyotiwa moto na mwokaji; huacha kuuchochea moto, tangu kuukanda unga hata umekwisha kutiwa chachu.
Jérémie 9.2 Osée 4.2 Osée 4.12 Jacques 4.4 Jérémie 5.7-5.8
5 Sikukuu ya mfalme wetu, wakuu walijitapisha kwa ukali wa divai; alinyosha mkono wake pamoja na wenye mzaha.
Esaïe 28.1 Esaïe 28.7-28.8 Esaïe 5.11-5.12 Proverbes 13.20 Psaumes 1.1
6 Maana wamefanya moyo wao kuwa tayari kama tanuu, wakati waoteapo; hasira yao hulala usiku kucha; asubuhi yawaka kama moto utoao miali.
Proverbes 4.16 Osée 7.4 2 Samuel 13.28-13.29 Osée 7.7 Michée 2.1
7 Wote wamepata moto kama tanuu, nao hula makadhi wao; wafalme wao wote wameanguka; hakuna hata mmoja wao aniitaye mimi.
2 Rois 15.14 2 Rois 15.25 2 Rois 15.10 2 Rois 15.30 Esaïe 64.7
8 Efraimu ajichanganya na mataifa; Efraimu ni mkate usiogeuzwa.
Psaumes 106.35 Osée 5.13 Matthieu 6.24 1 Rois 18.21 Malachie 2.11
9 Wageni wamekula nguvu zake, naye hana habari; naam, nywele za mvi zimeonekana huko na huko juu yake, naye hana habari.
Osée 8.7 Esaïe 57.1 Esaïe 42.22-42.25 Esaïe 1.7 2 Rois 13.22
10 Na kiburi cha Israeli chamshuhudia mbele ya uso wake; ila hata hivyo hawakumrudia Bwana, Mungu wao, wala hawakumtafuta kwa ajili ya hayo yote.
Osée 5.5 Esaïe 9.13 Amos 4.6-4.13 Psaumes 14.2 Jérémie 8.5-8.6
11 Naye Efraimu amekuwa kama njiwa mpumbavu, asiye na fahamu; humwita Misri, huenda Ashuru.
Osée 5.13 Osée 12.1 Osée 4.11 Osée 11.11 Osée 9.3
12 Watakapokwenda nitatandika wavu wangu juu yao; nitawashusha kama ndege wa angani; nitawarudi, kama vile mkutano wao ulivyosikia.
Ezéchiel 12.13 Deutéronome 28.15-28.68 2 Rois 17.13-17.18 Deutéronome 31.16-31.29 Deutéronome 29.22-29.28
13 Ole wao! Kwa kuwa wamenikimbia; uharibifu na uwapate! Kwa kuwa wameniasi; ingawa ninataka kuwakomboa, hata hivyo wamenena uongo juu yangu.
Osée 9.12 Osée 11.12 Ezéchiel 34.6 Psaumes 107.2-107.3 Michée 6.4
14 Wala hawakunililia kwa moyo, lakini wanalalamika vitandani mwao; hujikutanisha ili kupata nafaka na divai; huniasi mimi.
Amos 2.8 Job 35.9-35.10 Michée 2.11 Zacharie 7.5 Juges 9.27
15 Ingawa nimewafundisha na kuwatia nguvu mikono yao, hata hivyo hukusudia udhalimu juu yangu.
Nahum 1.9 Psaumes 94.12 Romains 1.21 Psaumes 62.3 Psaumes 106.43-106.45
16 Wao hurudi, lakini si kwake Aliye juu; wamekuwa kama upinde usiotumainika; wakuu wao wataanguka kwa upanga, kwa sababu ya jeuri ya ndimi zao; jambo hili litakuwa kwao sababu ya kuchekwa katika nchi ya Misri.
Psaumes 78.57 Osée 9.3 Psaumes 73.9 Ezéchiel 23.32 Psaumes 12.4

Cette Bible est dans le domaine public.