1 Na ahimidiwe Bwana, mwamba wangu, Anifundishaye mikono yangu vita, Vidole vyangu kupigana.Psaumes 18.34 Psaumes 18.2 2 Corinthiens 10.4 Deutéronome 32.30-32.31 Psaumes 44.3-44.4
2 Mhisani wangu na boma langu, Ngome yangu na mwokozi wangu, Ngao yangu niliyemkimbilia, Huwatiisha watu wangu chini yangu.
Psaumes 18.2 Psaumes 59.9 Psaumes 91.2 2 Samuel 22.2-22.3 Psaumes 18.47
3 Ee Bwana, mtu ni kitu gani hata umjue? Na binadamu hata umwangalie?
Psaumes 8.4 Hébreux 2.6 Job 7.17 Job 15.14 Psaumes 146.3-146.4
4 Binadamu amefanana na ubatili, Siku zake ni kama kivuli kipitacho.
Psaumes 102.11 Psaumes 109.23 Job 8.9 2 Samuel 14.14 Ecclésiaste 8.13
5 Bwana, uziinamishe mbingu zako, ushuke, Uiguse milima nayo itatoka moshi.
Psaumes 104.32 Psaumes 18.9 Habakuk 3.3-3.6 Hébreux 12.18 Exode 19.18
6 Utupe umeme, uwatawanye, Uipige mishale yako, uwafadhaishe.
Deutéronome 32.23 Psaumes 21.12 Psaumes 77.17-77.18 Deutéronome 32.42 Psaumes 18.13-18.14
7 Uinyoshe mikono yako toka juu, uniponye, Unitoe katika maji mengi, katika mkono wa wageni.
Psaumes 18.16 Psaumes 69.1-69.2 Psaumes 93.3-93.4 Apocalypse 17.15 2 Samuel 22.17
8 Vinywa vyao vyasema visivyofaa, Na mkono wao wa kuume ni mkono wa uongo.
Psaumes 12.2 Psaumes 41.6 Esaïe 44.20 Psaumes 109.2-109.3 Psaumes 62.4
9 Ee Mungu, nitakuimbia wimbo mpya, Kwa kinanda chenye nyuzi kumi nitakuimbia.
Psaumes 33.2-33.3 Psaumes 40.3 1 Chroniques 25.1-25.6 Psaumes 108.2-108.3 Psaumes 149.1
10 Awapaye wafalme wokovu, Amwokoa Daudi, mtumishi wake, na upanga wa uovu.
Psaumes 18.50 Psaumes 140.7 Psaumes 33.16-33.18 Esaïe 45.1-45.6 2 Samuel 21.16-21.17
11 Uniponye, unitoe, Katika mkono wa wageni. Vinywa vyao vyasema visivyofaa, Na mkono wao wa kuume ni mkono wa uongo.
2 Samuel 17.1-17.14 Esaïe 44.20 2 Samuel 16.5-16.14 2 Samuel 10.6-10.19 Psaumes 12.2
12 Wana wetu na wawe kama miche Waliokua ujanani. Binti zetu kama nguzo za pembeni Zilizonakishwa kwa kupamba hekalu.
Psaumes 128.3 Lamentations 4.2 Esaïe 44.3-44.5 Psaumes 127.4-127.5 Job 42.15
13 Ghala zetu na zijae Zenye akiba za jinsi zote. Kondoo zetu na wazae Elfu na makumi elfu mashambani mwetu.
Luc 12.16-12.20 Malachie 3.10 Lévitique 26.5 Genèse 30.29-30.31 Lévitique 26.10
14 Ng’ombe zetu na wachukue mizigo, Kusiwe na kushambuliwa. Wala kusiwe na kuhamishwa, Wala malalamiko katika njia zetu.
Jérémie 14.2 Jérémie 13.17-13.19 Lamentations 1.4-1.6 Zacharie 8.3-8.5 Deutéronome 28.7
15 Heri watu wenye hali hiyo, Heri watu wenye Bwana kuwa Mungu wao.
Psaumes 33.12 Deutéronome 33.29 Psaumes 146.5 Ephésiens 1.3 Psaumes 89.15