Jugement de Babylone
1 Haya, shuka, keti mavumbini, Ewe bikira, binti Babeli; Keti chini pasipo kiti cha enzi, Ewe binti wa Wakaldayo; Maana hutaitwa tena mwororo, mpenda anasa.
Psaumes 137.8 Zacharie 2.7 Jérémie 51.33 Jérémie 46.11 Esaïe 3.26
2 Twaa mawe ya kusagia, usage unga; Vua utaji wako, ondoa mavazi yako, Funua mguu wako, pita katika mito ya maji.
Matthieu 24.41 Juges 16.21 Exode 11.5 Job 31.10 Esaïe 20.4
3 Uchi wako utafunuliwa, Naam, aibu yako itaonekana. Nitalipa kisasi; simkubali mtu ye yote.
Nahum 3.5 Jérémie 51.20-51.24 Hébreux 10.30-10.31 Apocalypse 18.5-18.8 Esaïe 34.1-34.8
4 Mkombozi wetu, Bwana wa majeshi ndilo jina lake, Mtakatifu wa Israeli.
Esaïe 41.14 Esaïe 43.14 Esaïe 49.26 Jérémie 31.11 Esaïe 43.3
5 Kaa kimya, ingia gizani, Ee binti wa Wakaldayo; Maana hutaitwa tena Malkia wa falme.
Esaïe 47.7 Apocalypse 18.7 Daniel 2.37-2.38 Psaumes 46.10 1 Samuel 2.9
6 Nalikuwa nimekasirika na watu wangu, naliutia unajisi urithi wangu, nikawatia mkononi mwako; wewe hukuwatendea rehema; uliwatia wazee nira yako, nayo nzito sana.
Zacharie 1.15 2 Chroniques 28.9 Deutéronome 28.50 Abdias 1.16 Abdias 1.10
7 Ukasema, Mimi nitakuwa bibi milele; hata hukuyatia hayo moyoni mwako, wala hukukumbuka mwisho wa mambo hayo.
Deutéronome 32.29 Esaïe 47.5 Jérémie 5.31 Ezéchiel 7.3-7.9 Daniel 4.29
8 Sasa, basi, sikia haya, wewe upendaye anasa, ukaaye na kujiona salama, wewe usemaye moyoni mwako, Mimi ndiye, wala hapana mwingine zaidi yangu mimi; sitaketi mfano wa mjane, wala sitajua kufiwa na watoto;
Sophonie 2.15 Esaïe 32.9 Esaïe 45.6 Jérémie 50.11 Esaïe 47.10
9 lakini mambo haya mawili yatakupata katika dakika moja siku moja, kufiwa na watoto, na ujane; yatakupata kiasi kitimilifu, uchawi wako ujapokuwa mwingi, na uganga wako mwingi mno.
Nahum 3.4 1 Thessaloniciens 5.3 Psaumes 73.19 Esaïe 47.12-47.13 Apocalypse 18.8-18.10
10 Maana umeutumainia ubaya wako; umesema, Hapana anionaye; hekima yako, na maarifa yako yamekupotosha, nawe umesema moyoni mwako, Mimi ndiye, wala hapana mwingine zaidi yangu mimi.Psaumes 52.7 Esaïe 5.21 Esaïe 29.15 Ezéchiel 8.12 Ezéchiel 9.9
11 Kwa sababu hiyo ubaya utakupata; wala hutajua kutopoa kwake; na msiba utakuangukia; hutaweza kuuondoa; na ukiwa utakupata kwa ghafula, usioujua.
1 Thessaloniciens 5.3 Luc 12.59 Esaïe 37.36 Néhémie 4.11 Apocalypse 18.9-18.10
12 Simama sasa na uganga wako, na wingi wa uchawi wako, uliojitaabisha nao tangu ujana wako; labda utaweza kupata faida, labda utaweza kushinda.
Jérémie 2.28 Esaïe 47.9-47.10 Nahum 3.4 Daniel 5.7-5.9 Actes 13.8-13.12
13 Umechoka kwa wingi wa mashauri yako; basi, na wasimame hao wajuao falaki, wazitazamao nyota, watabirio kila mwezi mambo ya mwezi huo, wakakuokoe na mambo yatakayokupata.
Esaïe 44.25 Esaïe 57.10 Jérémie 51.58 Daniel 2.2-2.10 Ezéchiel 24.12
14 Tazama, watakuwa kama mabua makavu; moto utawateketeza; hawatajiokoa na nguvu za mwali wa moto; hautakuwa kaa la kukota moto, wala moto wa kukaa karibu nao.
Malachie 4.1 Nahum 1.10 Esaïe 41.2 Matthieu 10.28 Esaïe 10.17
15 Ndivyo yatakavyokuwa mambo hayo uliyojitaabisha nayo; wale waliofanya biashara nawe tangu ujana wako watatanga-tanga mbali nawe, kila mtu akienda zake; hapatakuwa na mtu wa kukuokoa.
Ezéchiel 27.12-27.25 Apocalypse 18.11-18.19 Esaïe 56.11 Jérémie 51.6-51.9