Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Cantique 5
Bible en Swahili de l’est


1 Naingia bustanini mwangu, umbu langu, bibi arusi, Nachuma manemane yangu na rihani, Nala sega la asali na asali yangu, Nanywa divai yangu na maziwa. Kaleni, rafiki zangu, kanyweni, Naam, nyweni sana, wapendwa wangu. Cantique 6.2 Jean 3.29 Jean 15.14-15.15 Cantique 4.16 Esaïe 61.11
2 Nalikuwa nimelala, lakini moyo wangu u macho, Sikiliza! Mpendwa wangu anabisha! Nifungulie, umbu langu, mpenzi wangu, Hua wangu, mkamilifu wangu, Kwa maana kichwa changu kimelowa umande, Nywele zangu zina manyunyu ya usiku. Cantique 2.14 Cantique 6.9 Cantique 8.7 Apocalypse 3.20 Cantique 5.11
3 Nimeivua kanzu yangu; niivaeje? Nimeitawadha miguu; niichafueje? Luc 11.7 Matthieu 25.5 Matthieu 26.38-26.43 Proverbes 22.13 Romains 7.22-7.23
4 Mpendwa wangu aliutia mkono wake tunduni, Na moyo wangu ukachomeka kwa ajili yake. 1 Jean 3.16-3.17 Genèse 43.30 2 Corinthiens 8.16 Cantique 1.4 Actes 16.14
5 Nikaondoka nimfungulie mpendwa wangu; Mikono yangu ilidondoza manemane, Na vidole vyangu matone ya manemane, Penye vipini vya komeo. Cantique 5.13 Cantique 3.6 2 Corinthiens 7.9-7.11 Cantique 4.13-4.14 Apocalypse 3.20
6 Nalimfungulia mpendwa wangu, Lakini mpendwa wangu amegeuka amepita; (Nimezimia nafsi yangu aliponena), Nikamtafuta, nisimpate, Nikamwita, asiniitikie. Cantique 5.2 Esaïe 57.16 Genèse 42.28 Lamentations 3.8 Psaumes 22.1-22.2
7 Walinzi wazungukao mjini waliniona, Wakanipiga na kunitia jeraha, Walinzi walindao kuta zake Wakaninyang’anya shela yangu. Cantique 3.3 Matthieu 21.33-21.41 Actes 5.40-5.41 2 Corinthiens 11.13 Jean 16.2
8 Nawasihi, enyi binti za Yerusalemu, Ninyi mkimwona mpendwa wangu, Ni nini mtakayomwambia? Ya kwamba nazimia kwa mapenzi. Cantique 2.7 Cantique 2.5 Psaumes 42.1-42.3 Psaumes 63.1-63.3 Galates 6.1-6.2
9 Mpendwa wa namna gani ni mpendwa wako, Wewe uliye mzuri katika wanawake, Mpendwa wa namna gani ni mpendwa wako, Hata wewe utusihi hivyo? Cantique 1.8 Cantique 6.1 Esaïe 53.2 Psaumes 45.13 Cantique 6.9-6.10
10 Mpendwa wangu ni mweupe, tena mwekundu, Mashuhuri miongoni mwa elfu kumi; Psaumes 45.2 Romains 9.5 Colossiens 1.18 Deutéronome 32.31 Philippiens 2.9-2.11
11 Kichwa chake ni kama dhahabu safi sana, Nywele zake ni za ukoka, nyeusi kama kunguru; Ephésiens 1.21-1.22 Apocalypse 1.14 Cantique 5.2 Daniel 7.9 Daniel 2.37-2.38
12 Macho yake ni kama hua penye vijito, Wakioga kwa maziwa, wakiikalia mito iliyojaa; Cantique 1.15 Cantique 4.1 Hébreux 4.13
13 Mashavu yake ni kama matuta ya rihani, Ambayo hufanyizwa manukato; Midomo yake ni kama nyinyoro, Inadondoza matone ya manemane; Cantique 1.10 Cantique 2.1 Cantique 6.2 Psaumes 27.4 Esaïe 50.4
14 Mikono yake ni kama mianzi ya dhahabu, lliyopambwa kwa zabarajadi; Kiwiliwili chake kama kazi ya pembe, Iliyonakishiwa kwa yakuti samawi; Exode 24.10 Esaïe 54.11 Psaumes 99.4 Esaïe 9.7 Exode 15.6
15 Miguu yake ni kama nguzo za marimari, Zilizowekwa juu ya misingi ya dhahabu; Sura yake ni kama Lebanoni, Ni bora mfano wa mierezi; 1 Rois 4.33 Cantique 7.4 Psaumes 92.12 Matthieu 28.3 Juges 13.6
16 Kinywa chake kimejaa maneno matamu, Ndiye mzuri sana pia pia. Ni huyu mpendwa wangu, ni huyu rafiki yangu, Enyi binti za Yerusalemu. Psaumes 45.2 Esaïe 9.6-9.7 Cantique 7.9 Galates 2.20 Cantique 2.1

Cette Bible est dans le domaine public.