1 Yeye asetaye vipande vipande amepanda juu mbele ya uso wako; zishike silaha, ilinde njia, vitie nguvu viuno vyako, uongeze uwezo wako sana.
Jérémie 51.20-51.23 Jérémie 25.9 Esaïe 14.6 Joël 3.9-3.11 Jérémie 50.23
2 Kwa maana Bwana anairudisha fahari ya Yakobo, kama fahari ya Israeli; maana watekao nyara wamewateka, na kuyaharibu matawi ya mizabibu yao.
Psaumes 80.12-80.13 Sophonie 3.11 Genèse 49.22-49.23 Jérémie 49.9 Esaïe 60.15
3 Ngao ya mashujaa wake imefanywa kuwa nyekundu, watu walio hodari wa vita wamevaa nguo nyekundu sana; magari ya vita yametameta kwa chuma cha pua siku ya kujitengeza kwake, na mikuki inatikiswa kwa namna ya kutisha.
Ezéchiel 23.14-23.15 Apocalypse 12.3 Zacharie 1.8 Zacharie 11.2 Zacharie 6.2
4 Magari ya vita yanafanya mshindo njiani, Yanasongana-songana katika njia kuu; Kuonekana kwake ni kama mienge, Yanakwenda upesi kama umeme.Jérémie 4.13 Esaïe 66.15 Nahum 3.2-3.3 Ezéchiel 26.10 Esaïe 37.24
5 Awakumbuka watu wake wenye heshima; Wanajikwaa katika mwendo wao; Wanafanya haraka waende ukutani; Nacho kitu cha kuwafunika kimewekwa tayari.
Jérémie 46.12 Esaïe 5.27 Nahum 3.18 Nahum 3.3 Jérémie 50.29
6 Malango ya mito yamefunguka, na jumba la mfalme limeyeyushwa.
Esaïe 45.1-45.2 2 Pierre 3.10-3.11
7 Husabu naye amefunuliwa, anachukuliwa, na wajakazi wake wanalia kama kwa sauti ya hua, wakipiga-piga vifua vyao.
Esaïe 59.11 Esaïe 38.14 Luc 23.48 Esaïe 32.12 Luc 23.27
8 Lakini Ninawi tokea zamani amekuwa kama ziwa la maji; ila hata sasa wanakimbia; Simameni! Simameni! Lakini hapana hata mmoja atazamaye nyuma.
Apocalypse 17.1 Apocalypse 17.15 Esaïe 47.13 Jérémie 50.16 Nahum 3.17
9 Chukueni nyara za fedha; Chukueni nyara za dhahabu; Kwa maana ni akiba isiyoisha, Fahari ya vyombo vipendezavyo.
Jérémie 25.34 Ezéchiel 26.12 Daniel 11.8 Jérémie 51.56 2 Chroniques 36.10
10 Amekuwa utupu, na ukiwa, na uharibifu; hata moyo unayeyuka, na magoti yanagongana-gongana; viunoni mwote mna utungu, na nyuso za wote zimekuwa nyeupe kwa hofu.
Joël 2.6 Psaumes 22.14 Daniel 5.6 Esaïe 13.7-13.8 Sophonie 2.13-2.15
11 Kao la simba li wapi? Na mahali walishapo wana-simba pa wapi, mahali walipotembea simba mume na simba mke na mwana-simba, wala hapana aliyewatia hofu?
Esaïe 5.29 Jérémie 2.15 Esaïe 31.4 Ezéchiel 19.2-19.8 Jérémie 50.17
12 Simba alirarua vipande vipande chakula cha kuwatosha watoto wake, aliwasongea wake zake nyama, aliyajaza mapango yake mateka, na makao yake aliyajaza mawindo.
Jérémie 51.34 Esaïe 10.6-10.14 Psaumes 17.12
13 Tazama, mimi ni juu yako, asema Bwana wa majeshi, nami nitayateketeza magari yako ya vita katika moshi, na upanga utawala wana-simba wako; nami nitayakatilia mbali mawindo yako katika nchi, na sauti za wajumbe wako hazitasikiwa tena kamwe.
Psaumes 46.9 2 Rois 19.23 Nahum 3.5 Jérémie 21.13 Nahum 3.1