Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Corinthiens 13
Bible en Swahili de l’est


1 Hii ndiyo mara ya tatu ya mimi kuja kwenu. Kwa vinywa vya mashahidi wawili au watatu kila neno litathibitishwa. Deutéronome 19.15 2 Corinthiens 12.14 Matthieu 18.16 Deutéronome 17.6 Nombres 35.30
2 Nimetangulia kuwaambia; na, kama vile nilipokuwapo mara ya pili, vivyo hivyo sasa nisipokuwapo, nawaambia wazi wao waliotenda dhambi tangu hapo, na wengine wote, ya kwamba, nikija, sitahurumia; 2 Corinthiens 1.23 1 Corinthiens 5.5 2 Corinthiens 10.8-10.11 1 Corinthiens 4.19-4.21 2 Corinthiens 10.1-10.2
3 kwa kuwa mnatafuta dalili ya Kristo, asemaye ndani yangu, ambaye si dhaifu kwenu, bali ana uweza ndani yenu. Matthieu 10.20 2 Corinthiens 12.12 2 Corinthiens 2.10 1 Corinthiens 5.4-5.5 2 Corinthiens 2.6
4 Maana, alisulibiwa katika udhaifu, lakini anaishi kwa nguvu za Mungu. Maana sisi nasi tu dhaifu katika yeye; lakini tutaishi pamoja naye kwa uweza wa Mungu ulio kwenu. 1 Pierre 3.18 Romains 6.4 Romains 1.4 1 Corinthiens 2.3 Jean 10.18
5 Jijaribuni wenyewe kwamba mmekuwa katika imani; jithibitisheni wenyewe. Au hamjijui wenyewe, kwamba Yesu Kristo yu ndani yenu? Isipokuwa mmekataliwa. 1 Corinthiens 11.28 Lamentations 3.40 1 Corinthiens 9.27 Hébreux 12.15 Galates 6.4
6 Lakini natumaini kama mtajua ya kuwa sisi hatukukataliwa. 2 Corinthiens 13.3-13.4 2 Corinthiens 13.10 2 Corinthiens 12.20
7 Nasi twamwomba Mungu, msifanye lo lote lililo baya; si kwamba sisi tuonekane tumekubaliwa, lakini ninyi mfanye lile lililo jema, tujapokuwa sisi tu kama waliokataliwa. 1 Timothée 2.2 Jacques 1.12 1 Pierre 2.12 2 Timothée 2.15 2 Timothée 4.18
8 Maana hatuwezi kutenda neno lo lote kinyume cha kweli, bali kwa ajili ya kweli. 1 Timothée 1.20 Actes 4.28-4.30 Actes 19.11-19.17 Luc 9.49-9.56 2 Corinthiens 13.10
9 Maana twafurahi, iwapo sisi tu dhaifu, nanyi mmekuwa hodari. Tena twaomba hili nalo, kutimilika kwenu. 2 Corinthiens 13.11 1 Thessaloniciens 3.10 1 Corinthiens 4.10 Hébreux 12.23 Ephésiens 4.12-4.13
10 Kwa sababu hiyo, naandika haya nisipokuwapo, ili, nikiwapo, nisiutumie ukali kwa kadiri ya uwezo ule niliopewa na Bwana, kwa kujenga wala si kwa kubomoa. 2 Corinthiens 10.8 2 Corinthiens 2.3 Tite 1.13 2 Corinthiens 12.20-12.21 2 Corinthiens 13.8
11 Hatimaye, ndugu, kwaherini; mtimilike, mfarijike, nieni mamoja, mkae katika amani; na Mungu wa upendo na amani atakuwa pamoja nanyi. Romains 15.33 Marc 9.50 Romains 12.16 1 Corinthiens 1.10 Romains 12.18
12 Salimianeni kwa busu takatifu. Romains 16.16 1 Pierre 5.14 1 Corinthiens 16.20 1 Thessaloniciens 5.26
13 Watakatifu wote wawasalimu. 2 Jean 1.13 Romains 16.21-16.23 Philémon 1.23-1.24 Hébreux 13.24 3 Jean 1.14
14 Neema ya Bwana Yesu Kristo, na pendo la Mungu, na ushirika wa Roho Mtakatifu ukae nanyi nyote. Romains 16.20 Philippiens 2.1 Romains 5.5 Jude 1.21 Romains 8.14-8.17

Cette Bible est dans le domaine public.