1 Basi, ndugu, tunakusihini, kwa habari ya kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo, na kukusanyika kwetu mbele zake,
Marc 13.27 Matthieu 24.31 1 Thessaloniciens 4.14-4.17 1 Thessaloniciens 2.19 Romains 12.1
2 kwamba msifadhaishwe upesi hata kuiacha nia yenu, wala msisitushwe, kwa roho, wala kwa neno, wala kwa waraka unaodhaniwa kuwa ni wetu, kana kwamba siku ya Bwana imekwisha kuwapo.
1 Jean 4.1-4.2 1 Corinthiens 1.8 Marc 13.7 Jérémie 23.25-23.27 1 Thessaloniciens 3.3
3 Mtu awaye yote asiwadanganye kwa njia yo yote; maana haiji, usipokuja kwanza ule ukengeufu; akafunuliwa yule mtu wa kuasi, mwana wa uharibifu;
Ephésiens 5.6 Daniel 7.25 Matthieu 24.4-24.6 Jean 17.12 1 Timothée 4.1-4.3
4 yule mpingamizi, ajiinuaye nafsi yake juu ya kila kiitwacho Mungu ama kuabudiwa; hata yeye mwenyewe kuketi katika hekalu la Mungu, akijionyesha nafsi yake kana kwamba yeye ndiye Mungu.
Ezéchiel 28.2 1 Corinthiens 8.5 Apocalypse 13.6-13.7 Esaïe 14.13-14.14 Daniel 8.9-8.14
5 Je! Hamkumbuki ya kuwa wakati nilipokuwapo pamoja nanyi naliwaambieni hayo?2 Thessaloniciens 3.10 Actes 20.31 Luc 24.6-24.7 2 Pierre 1.15 Matthieu 16.9
6 Na sasa lizuialo mwalijua, yule apate kufunuliwa wakati wake.
2 Thessaloniciens 2.3 2 Thessaloniciens 2.8
7 Maana ile siri ya kuasi hivi sasa inatenda kazi; lakini yuko azuiaye sasa, hata atakapoondolewa.
1 Jean 2.18 Apocalypse 17.7 Apocalypse 17.5 1 Jean 4.3 Colossiens 2.18-2.23
8 Hapo ndipo atakapofunuliwa yule asi, ambaye Bwana Yesu atamwua kwa pumzi ya kinywa chake, na kumwangamiza kwa ufunuo wa kuwapo kwake;
Esaïe 11.4 Apocalypse 19.15 2 Thessaloniciens 2.3 Daniel 7.10-7.11 Apocalypse 2.16
9 yule ambaye kuja kwake ni kwa mfano wa kutenda kwake Shetani, kwa uwezo wote, na ishara na ajabu za uongo;
Matthieu 24.24 Apocalypse 18.23 Apocalypse 19.20 Deutéronome 13.1-13.2 2 Timothée 3.8
10 na katika madanganyo yote ya udhalimu kwa hao wanaopotea; kwa sababu hawakukubali kuipenda ile kweli, wapate kuokolewa.
Proverbes 1.7 1 Corinthiens 1.18 2 Corinthiens 4.2-4.3 1 Corinthiens 16.22 2 Pierre 2.12
11 Kwa hiyo Mungu awaletea nguvu ya upotevu, wauamini uongo;
Romains 1.28 Ezéchiel 14.9 Jérémie 27.10 Ezéchiel 21.29 Esaïe 6.9-6.10
12 ili wahukumiwe wote ambao hawakuiamini kweli, bali walikuwa wakijifurahisha katika udhalimu.
Romains 1.32 Romains 2.8 Romains 8.7-8.8 Marc 16.16 Psaumes 50.16-50.21
13 Lakini imetupasa sisi kumshukuru Mungu sikuzote kwa ajili yenu, ndugu mliopendwa na Bwana, kwa kuwa Mungu amewachagua tangu mwanzo mpate wokovu, katika kutakaswa na Roho, na kuiamini kweli;
2 Timothée 1.9 1 Thessaloniciens 1.4 Actes 13.48 2 Thessaloniciens 1.3 1 Thessaloniciens 5.9
14 aliyowaitia ninyi kwa injili yetu, ili kuupata utukufu wa Bwana wetu Yesu Kristo.
1 Thessaloniciens 2.12 1 Pierre 5.10 1 Thessaloniciens 1.5 Romains 8.28-8.30 Matthieu 25.21
15 Basi, ndugu, simameni imara, mkayashike mapokeo mliyofundishwa, ama kwa maneno, ama kwa waraka wetu.
1 Corinthiens 11.2 2 Thessaloniciens 2.2 2 Thessaloniciens 3.6 1 Corinthiens 16.13 Jude 1.3
16 Na Bwana wetu Yesu Kristo mwenyewe, na Mungu Baba yetu, aliyetupenda akatupa faraja ya milele na tumaini jema, katika neema,
Jean 3.16 1 Pierre 1.3-1.8 Ephésiens 5.25 1 Thessaloniciens 3.11 Jean 14.16-14.18
17 awafariji mioyo yenu, na kuwafanya imara katika kila neno na tendo jema.
2 Thessaloniciens 3.3 1 Thessaloniciens 3.2 1 Thessaloniciens 3.13 2 Corinthiens 1.3-1.6 2 Thessaloniciens 2.16