Maladie et guérison d’Ézéchias
1 Siku hizo Hezekia aliugua, akawa katika hatari ya kufa; na Isaya nabii, mwana wa Amozi, akaenda kwa mfalme, akamwambia, Bwana asema hivi, Tengeneza mambo ya nyumba yako; maana utakufa, wala hutapona.
2 Samuel 17.23 2 Chroniques 32.24 2 Rois 20.1-20.11 Esaïe 38.1-38.8 Jonas 3.4
2 Basi Hezekia akajigeuza, akaelekeza uso wake ukutani, akamwomba Bwana,
Psaumes 50.15 Matthieu 6.6 1 Rois 8.30 Psaumes 91.15
3 akasema, Ee Bwana, kumbuka haya, nakusihi, kwamba nimekwenda mbele zako katika kweli na kwa moyo mkamilifu, na kutenda yaliyo mema machoni pako. Hezekia akalia sana sana.
Néhémie 13.14 1 Chroniques 29.19 Psaumes 6.8 Psaumes 32.2 2 Chroniques 31.20-31.21
4 Ikawa, neno la Bwana likamjia Isaya, kusema,
5 Enenda ukamwambie Hezekia, Bwana, Mungu wa Daudi, baba yako, asema hivi, Mimi nimeyasikia maombi yako, nimeyaona machozi yako; tazama, nitaziongeza siku zako, kiasi cha miaka kumi na mitano.
2 Rois 18.2 Psaumes 89.3-89.4 1 Rois 9.4-9.5 1 Rois 15.4 2 Rois 19.20
6 Nami nitakuokoa wewe, na mji huu, na mkono wa mfalme wa Ashuru, nami nitaulinda mji huu.
Esaïe 37.35 2 Timothée 4.17 Esaïe 31.4-31.5 Esaïe 12.6 2 Chroniques 32.22
7 Jambo hili liwe ishara kwako, itokayo kwa Bwana, ya kuwa Bwana atalitimiza jambo hili alilolisema;
Juges 6.37-6.39 Esaïe 37.30 2 Rois 20.8-20.21 Esaïe 38.22 Esaïe 7.11-7.14
8 Tazama, nitakirudisha nyuma kivuli madaraja kumi, ambayo kilishuka juu ya duara ya Ahazi kwa sababu ya jua. Basi jua likarudi madaraja kumi katika hiyo duara, ambayo limekwisha kushuka.
Matthieu 16.1 2 Chroniques 32.24 2 Rois 20.9-20.11 2 Chroniques 32.31 Josué 10.12-10.14
9 Haya ndiyo maandiko ya Hezekia, mfalme wa Yuda, alipokuwa hawezi, naye akapona ugonjwa wake.
Exode 15.1-15.21 Osée 6.1-6.2 Juges 5.1-5.31 Psaumes 118.18-118.19 1 Samuel 2.1-2.10
10 Nalisema, Katika usitawi wa siku zangu nitakwenda kuingia malango ya kuzimu; Nimenyimwa mabaki ya miaka yangu.
2 Corinthiens 1.9 Psaumes 102.24 Esaïe 38.1 Job 7.7 Psaumes 107.18
11 Nalisema, Sitamwona Bwana, yeye Bwana, katika nchi ya walio hai; Sitamwona mwanadamu tena pamoja na hao wakaao duniani.
Psaumes 27.13 Psaumes 31.22 Ecclésiaste 9.5-9.6 Psaumes 6.4-6.5 Psaumes 116.8-116.9
12 Kao langu limeondolewa kabisa, limechukuliwa kama hema ya mchungaji; Nimekunja maisha yangu kama mfumaji; atanikatilia mbali na kitanda cha mfumi; Tangu mchana hata usiku wanimaliza.
2 Corinthiens 5.1 Hébreux 1.12 Psaumes 73.14 Psaumes 31.22 Esaïe 1.8
13 Nalijituliza hata asubuhi; kama simba, aivunja mifupa yangu yote; Tangu mchana hata usiku wanimaliza.
Psaumes 51.8 Daniel 6.24 Psaumes 50.22 1 Rois 13.24-13.26 Psaumes 39.10
14 Kama mbayuwayu au korongo ndivyo nilivyolia; Naliomboleza kama hua; macho yangu yamedhoofu kwa kutazama juu; Ee Bwana, nimeonewa, na uwe mdhamini wangu.
Esaïe 59.11 Job 30.29 Nahum 2.7 Psaumes 69.3 Ezéchiel 7.16
15 Niseme nini? Yeye amenena nami, na yeye mwenyewe ametenda hayo; Nitakwenda polepole miaka yangu yote, kwa sababu ya uchungu wa nafsi yangu.
1 Rois 21.27 Job 7.11 Job 10.1 2 Rois 4.27 Josué 7.8
16 Ee Bwana, kwa mambo hayo watu huishi; Na uhai wa roho yangu u katika hayo yote; Kwa hiyo uniponye na kunihuisha.
Deutéronome 8.3 Esaïe 64.5 1 Corinthiens 11.32 Job 33.19-33.28 Hébreux 12.10-12.11
17 Tazama; nalikuwa na uchungu mwingi kwa ajili ya amani yangu; Lakini kwa kunipenda umeniokoa na shimo la uharibifu; Kwa maana umezitupa dhambi zangu zote nyuma yako.
Esaïe 43.25 Jérémie 31.34 Psaumes 30.3 Jonas 2.6 Psaumes 86.13
18 Kwa kuwa kuzimu hakuwezi kukusifu; mauti haiwezi kukuadhimisha; Wale washukao shimoni hawawezi kuitarajia kweli yako.
Ecclésiaste 9.10 Psaumes 30.9 Psaumes 6.5 Nombres 16.33 Luc 16.26-16.31
19 Aliye hai, naam, aliye hai, ndiye atakayekusifu, kama mimi leo; Baba atawajulisha watoto kweli yako.Deutéronome 6.7 Deutéronome 4.9 Psaumes 78.3-78.6 Josué 4.21-4.22 Psaumes 119.175
20 Bwana yu tayari kunipa wokovu. Basi, kwa vinubi tutaziimba nyimbo zangu, Siku zote za maisha yetu nyumbani mwa Bwana.
Psaumes 30.11-30.12 Psaumes 51.15 Psaumes 68.25 Psaumes 27.5-27.6 Psaumes 116.17-116.19
21 Maana Isaya amesema, Na watwae mkate wa tini, wakauweke juu ya jipu, naye atapona.
Marc 7.33 2 Rois 20.7-20.8 Jean 9.6
22 Tena Hezekia alikuwa amesema, Iko ishara gani ya kunionyesha ya kuwa nitapanda niingie nyumbani mwa Bwana?
Psaumes 122.1 2 Rois 20.8 Psaumes 42.1-42.2 Psaumes 84.10-84.12 Psaumes 84.1-84.2