1 Roho yangu imezimika, siku zangu zimekoma, Kaburi i tayari kunipokea.
Psaumes 88.3-88.5 Esaïe 38.10-38.14 Job 19.17 Job 42.16 Job 6.11
2 Ni kweli wako kwangu wenye kufanya dhihaka, Jicho langu hukaa katika kunifanyia uchungu kwao.
1 Samuel 1.6-1.7 Job 16.20 Job 12.4 Job 21.3 Psaumes 35.14-35.16
3 Nipe rehani basi, uwe dhamana kwa ajili yangu kwako wewe mwenyewe; Kuna nani atakayeniwekea dhamana?
Proverbes 11.15 Proverbes 20.16 Psaumes 119.122 Esaïe 38.14 Hébreux 7.22
4 Kwani mioyo yao imeificha ufahamu; Kwa hiyo hutawakuza.
2 Chroniques 25.16 Romains 11.8 2 Samuel 15.31 Matthieu 11.25 1 Corinthiens 1.20
5 Awafitiniye rafiki zake wawe mawindo, Hata macho ya watoto wake yataingia kiwi.
Job 11.20 Psaumes 12.2-12.3 Job 32.21-32.22 1 Rois 11.12 Proverbes 20.19
6 Amenifanya niwe simo kwa watu; Nimekuwa mwenye kuchukiwa kwa wazi.
Job 30.9 Psaumes 44.14 Genèse 31.27 Esaïe 5.12 1 Rois 9.7
7 Jicho langu nalo limekuwa giza kwa sababu ya majonzi, Na via vyangu vyote vimekuwa kama kivuli.
Job 16.16 Psaumes 6.7 Lamentations 5.17 Psaumes 31.9-31.10 Psaumes 109.23
8 Walekevu watayastaajabia hayo, Na asiye na hatia atajiamsha juu ya mpotovu.
Romains 11.33 Habakuk 1.13 Actes 13.46 Psaumes 73.12-73.15 Job 22.19
9 Lakini mwenye haki ataishika njia yake, Naye mwenye mikono safi atazidi kupata nguvu.
Proverbes 4.18 Job 22.30 1 Jean 2.19 Esaïe 40.29-40.31 2 Corinthiens 12.9-12.10
10 Lakini rudini; ninyi nyote, njoni sasa; Wala sitampata mtu mwenye hekima kati yenu.
Job 6.29 Job 42.7 1 Corinthiens 1.20 Job 15.9 Job 17.4
11 Siku zangu zimepita, makusudi yangu yamevunjika, Hata hayo niliyo nayo moyoni mwangu.
Job 7.6 2 Corinthiens 1.15-1.17 Ecclésiaste 9.10 Proverbes 19.21 Lamentations 3.37
12 Wabadili usiku kuwa mchana; Wasema, Mwanga u karibu kwa sababu ya giza.
Deutéronome 28.67 Job 7.13-7.14 Job 7.3-7.4 Job 24.14-24.16
13 Nikitazamia kuzimu kuwa nyumba yangu; Nikitandika malazi yangu gizani;
Lamentations 3.25-3.26 Job 14.14 Job 30.23 Job 17.1 Psaumes 139.8
14 Ikiwa nimeuita uharibifu, Wewe u baba yangu; Na kuliambia buu, Wewe u mama yangu, na umbu langu;
Psaumes 16.10 Job 13.28 Job 21.26 1 Corinthiens 15.42 Job 21.32-21.33
15 Basi, tumaini langu li wapi? Na tumaini langu, ni nani atakayeliona?Job 13.15 Job 19.10 Job 7.6 Job 6.11 Job 4.6
16 Litashuka kwenye makomeo ya kuzimu, Itakapokuwapo raha mavumbini.
Job 3.17-3.19 Jonas 2.6 Psaumes 143.7 Job 33.18-33.28 Job 18.13-18.14