Hymne à la puissance et à la bonté de Dieu
1 Ee Mungu wangu, Mfalme, nitakutukuza, Nitalihimidi jina lako milele na milele.
Psaumes 30.1 Psaumes 95.3 Daniel 4.37 Esaïe 33.22 Psaumes 45.6
2 Kila siku nitakuhimidi, Nitalisifu jina lako milele na milele.
Psaumes 119.164 Psaumes 72.15 Psaumes 71.6 Apocalypse 7.15
3 Bwana ndiye mkuu mwenye kusifiwa sana, Wala ukuu wake hautambulikani.
Job 5.9 Job 9.10 Psaumes 147.5 Romains 11.33 Psaumes 139.6
4 Kizazi kwa kizazi kitayasifu matendo yako, Kitayatangaza matendo yako makuu.
Esaïe 38.19 Josué 4.21-4.24 Psaumes 71.18 Psaumes 44.1-44.2 Psaumes 78.3-78.7
5 Nitaifikiri fahari ya utukufu wa adhama yako, Na matendo yako yote ya ajabu.
Daniel 4.37 Psaumes 96.3 Psaumes 119.27 Psaumes 72.18 Psaumes 40.9-40.10
6 Watu watayataja matendo yako ya kutisha, Nami nitausimulia ukuu wako.
Daniel 3.28-3.29 Psaumes 107.31-107.32 Daniel 6.25-6.27 Psaumes 22.31 Josué 9.9-9.10
7 Watalihubiri kumbukumbu la wema wako mkuu. Wataiimba haki yako.
Esaïe 63.7 Psaumes 51.14 Psaumes 71.19 1 Pierre 2.9-2.10 Matthieu 12.34-12.35
8 Bwana ana fadhili, ni mwingi wa huruma, Si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa rehema,
Nombres 14.18 Psaumes 86.5 Psaumes 86.15 Psaumes 100.5 Exode 34.6-34.7
9 Bwana ni mwema kwa watu wote, Na rehema zake zi juu ya kazi zake zote.
Nahum 1.7 Psaumes 100.5 Jonas 4.11 Actes 14.17 Psaumes 36.6-36.7
10 Ee Bwana, kazi zako zote zitakushukuru, Na wacha Mungu wako watakuhimidi.
Psaumes 19.1 Psaumes 103.22 Psaumes 97.12 Psaumes 68.26 1 Pierre 2.9
11 Wataunena utukufu wa ufalme wako, Na kuuhadithia uweza wako.
Psaumes 45.6-45.7 1 Chroniques 29.11-29.12 Marc 11.9-11.10 Matthieu 6.13 Zacharie 9.9
12 Ili kuwajulisha watu matendo yake makuu, Na utukufu wa fahari ya ufalme wake.
Psaumes 105.1 Ephésiens 1.19-1.21 Psaumes 145.6-145.12 Psaumes 106.2 Daniel 4.34-4.35
13 Ufalme wako ni ufalme wa zamani zote, Na mamlaka yako ni ya vizazi vyote.1 Timothée 1.17 1 Corinthiens 15.21-15.28 Daniel 2.44 Psaumes 10.16 Daniel 7.27
14 Bwana huwategemeza wote waangukao, Huwainua wote walioinama chini.
Psaumes 146.8 Psaumes 37.24 Luc 22.31-22.32 Psaumes 38.6 Luc 13.11-13.13
15 Macho ya watu wote yakuelekea Wewe, Nawe huwapa chakula chao wakati wake.
Psaumes 104.27 Psaumes 136.25 Psaumes 147.8-147.9 Actes 17.25 Job 38.39-38.41
16 Waufumbua mkono wako, Wakishibisha kila kilicho hai matakwa yake.
Psaumes 104.28 Psaumes 132.15 Psaumes 107.9 Job 38.27
17 Bwana ni mwenye haki katika njia zake zote, Na mwenye fadhili juu ya kazi zake zote.
Deutéronome 32.4 Psaumes 99.3-99.4 Romains 3.5-3.6 Psaumes 97.2 Zacharie 9.9
18 Bwana yu karibu na wote wamwitao, Wote wamwitao kwa uaminifu.
Psaumes 34.18 Deutéronome 4.7 Jean 4.24 Jérémie 29.12-29.13 Esaïe 58.9
19 Atawafanyia wamchao matakwa yao, Naye atakisikia kilio chao na kuwaokoa.
Jean 15.7 Psaumes 37.4 Proverbes 15.29 1 Jean 5.15 Jean 16.24
20 Bwana huwahifadhi wote wampendao, Na wote wasio haki atawaangamiza.
Psaumes 97.10 Psaumes 31.23 Romains 8.28-8.30 Psaumes 9.17 Psaumes 37.28
21 Kinywa changu kitazinena sifa za Bwana; Wote wenye mwili na walihimidi jina lake takatifu milele na milele.
Psaumes 71.8 Psaumes 150.6 Psaumes 145.1-145.2 Psaumes 51.15 Psaumes 103.22