1 Mungu, Mungu Bwana, amenena, ameiita nchi, Toka maawio ya jua hata machweo yake.
Psaumes 113.3 Josué 22.22 Matthieu 25.32 1 Chroniques 15.17 1 Rois 18.21
2 Tokea Sayuni, ukamilifu wa uzuri, Mungu amemulika.
Deutéronome 33.2 Psaumes 48.2 Psaumes 80.1 Zacharie 9.17 Esaïe 12.6
3 Mungu wetu atakuja wala hatanyamaza, Moto utakula mbele zake, na tufani yavuma sana ikimzunguka pande zote.
Daniel 7.10 Lévitique 10.2 Nombres 16.35 Nahum 1.5-1.7 Hébreux 10.28-10.29
4 Ataziita mbingu zilizo juu, Na nchi pia awahukumu watu wake.
Esaïe 1.2 Deutéronome 32.1 Deutéronome 31.28 Michée 6.1-6.2 Deutéronome 4.26
5 Nikusanyieni wacha Mungu wangu Waliofanya agano nami kwa dhabihu.
Hébreux 12.24 Matthieu 26.28 1 Thessaloniciens 3.13 Hébreux 9.10-9.23 Hébreux 13.20
6 Na mbingu zitatangaza haki yake, Kwa maana Mungu ndiye aliye hakimu.Psaumes 75.7 Psaumes 97.6 Psaumes 89.5 Apocalypse 19.2 Romains 2.5
7 Sikieni, enyi watu wangu, nami nitanena, Mimi nitakushuhudia, Israeli; Mimi ndimi niliye MUNGU, Mungu wako.
Psaumes 81.8 Exode 20.2 Néhémie 9.29-9.30 Ezéchiel 20.7 Psaumes 81.10-81.12
8 Sitakukemea kwa ajili ya dhabihu zako, Na kafara zako ziko mbele zangu daima.
Hébreux 10.4-10.10 Psaumes 40.6-40.8 Osée 6.6 Esaïe 1.11-1.31 Psaumes 51.16
9 Sitatwaa ng’ombe katika nyumba yako, Wala beberu katika mazizi yako.
Psaumes 69.31 Actes 17.25 Michée 6.6-6.8 Esaïe 43.23-43.24 Hébreux 10.4-10.6
10 Maana kila hayawani ni wangu, Na makundi juu ya milima elfu.
Genèse 31.9 Genèse 1.24-1.25 Jonas 4.11 Jérémie 27.5-27.6 Psaumes 8.6-8.8
11 Nawajua ndege wote wa milima, Na wanyama wote wa mashamba ni wangu
Matthieu 6.26 Genèse 1.20-1.22 Ezéchiel 14.15-14.16 Psaumes 147.9 Job 39.26-39.30
12 Kama ningekuwa na njaa singekuambia, Maana ulimwengu ni wangu, navyo viujazavyo.
Exode 19.5 Deutéronome 10.14 Psaumes 145.15-145.16 Genèse 8.17 Genèse 1.11-1.12
13 Je! Nile nyama ya mafahali! Au ninywe damu ya mbuzi!
14 Mtolee Mungu dhabihu za kushukuru; Mtimizie Aliye juu nadhiri zako.
Deutéronome 23.21 Hébreux 13.15 Psaumes 56.12 Psaumes 116.12-116.14 Psaumes 107.21-107.22
15 Ukaniite siku ya mateso; Nitakuokoa, na wewe utanitukuza.
Psaumes 107.28 Psaumes 91.15 Psaumes 81.7 Zacharie 13.9 Psaumes 107.19
16 Bali mtu asiye haki, Mungu amwambia, Una nini wewe kuitangaza sheria yangu, Na kuliweka agano langu kinywani mwako?
Psaumes 78.36-78.38 Esaïe 1.11-1.15 Hébreux 8.9 Esaïe 48.1-48.2 Psaumes 25.14
17 Maana wewe umechukia maonyo, Na kuyatupa maneno yangu nyuma yako.
Néhémie 9.26 Proverbes 12.1 Proverbes 1.7 Jérémie 8.9 Romains 2.21-2.23
18 Ulipomwona mwivi ulikuwa radhi naye, Ukashirikiana na wazinzi.
Romains 1.32 1 Timothée 5.22 Job 31.9-31.11 Proverbes 1.10-1.19 Matthieu 23.30
19 Umekiachia kinywa chako kinene mabaya, Na ulimi wako watunga hila.
Psaumes 10.7 Psaumes 55.21 Osée 4.2 Esaïe 59.3-59.4 Romains 3.13-3.14
20 Umekaa na kumsengenya ndugu yako, Na mwana wa mama yako umemsingizia.
Matthieu 10.21 Matthieu 5.11 Lévitique 19.16 Tite 2.3 Proverbes 10.18
21 Ndivyo ulivyofanya, nami nikanyamaza; Ukadhani ya kuwa Mimi ni kama wewe. Walakini nitakukemea; Nitayapanga hayo mbele ya macho yako.
Psaumes 90.8 Esaïe 57.11 Ecclésiaste 8.11-8.12 Romains 2.4-2.5 Proverbes 29.1
22 Yafahamuni hayo, Ninyi mnaomsahau Mungu, Nisije nikawararueni, Asipatikane mwenye kuwaponya.
Psaumes 7.2 Psaumes 9.17 Job 8.13 Jérémie 2.32 Deutéronome 32.18
23 Atoaye dhabihu za kushukuru, Ndiye anayenitukuza. Naye autengenezaye mwenendo wake, Nitamwonyesha wokovu wa Mungu.
Psaumes 91.16 Jacques 3.13 Actes 13.26 Jean 7.17 Jean 8.31-8.32