Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Job 13
Bible en Swahili de l’est


1 Tazama, jicho langu limeyaona hayo yote, Sikio langu limeyasikia na kuelewa nayo.
Job 8.8-8.10 Job 5.9-5.16 Psaumes 78.3-78.4 Job 42.3-42.6 Job 15.17-15.18
2 Hayo myajuayo ninyi, na mimi pia nayajua; Mimi si duni kuliko ninyi.
Job 12.3 Job 42.7 2 Corinthiens 12.11 Job 34.35 Job 37.2
3 Hakika ningenena naye huyo Mwenyezi, Nami nataka kuhojiana na Mungu.
Esaïe 41.21 Job 31.35 Job 9.3 Job 13.22 Job 9.34-9.35
4 Lakini ninyi hubuni maneno ya uongo, Ninyi nyote ni matabibu wasiofaa.
Psaumes 119.69 Jérémie 46.11 Job 16.2 Jérémie 8.22 Job 6.21
5 Laiti mngenyamaza kabisa! Hilo lingekuwa hekima kwenu.
Proverbes 17.28 Jacques 1.19 Ecclésiaste 5.3 Job 13.13 Job 11.3
6 Sikieni sasa basi hoja zangu, Mkayasikie mashindano ya midomo yangu.
Proverbes 8.6-8.7 Job 34.2 Job 21.2-21.3 Job 33.1-33.3 Juges 9.7
7 Je! Mtanena yasiyo ya haki kwa ajili ya Mungu, Na kusema kwa udanganyifu kwa ajili yake?
Job 36.4 Jean 16.2 Job 27.4 Job 32.21-32.22 2 Corinthiens 4.2
8 Je! Mtamwonyesha yeye upendeleo? Mtamtetea Mungu?
Proverbes 24.23 Job 34.19 Exode 23.2-23.3 Lévitique 19.15 Malachie 2.9
9 Je! Itafaa yeye kuwatafuta ninyi? Au, kama kumdanganya mtu, je! Mtamdanganya yeye?
Galates 6.7-6.8 Jérémie 17.10 Psaumes 139.23 Psaumes 44.21 Job 17.2
10 Hakika atawakemea ninyi, Mkiwapendelea watu kwa siri.
Jacques 2.9 Psaumes 50.21-50.22 Psaumes 82.2 Job 42.7-42.8
11 Je! Huo ukuu wake hautawatia hofu, Na utisho wake hautawaangukia?
Psaumes 119.120 Job 31.23 Esaïe 8.13 Matthieu 10.28 Apocalypse 15.3-15.4
12 Matamko yenu ya hekima ni mithali ya majivu, Ngome zenu ni ngome za udongo.
Proverbes 10.7 Genèse 18.27 Exode 17.14 Esaïe 26.14 Job 4.19
13 Nyamazeni, niacheni, ili nipate kunena, Na hayo yatakayonijilia na yaje.
Job 13.5 Job 7.11 Job 7.15-7.16 Job 21.3 Job 6.9-6.10
14 Nitaitwaa nyama ya mwili wangu katika meno yangu, Na kuutwaa uhai wangu mkononi mwangu!
Juges 12.3 1 Samuel 28.21 1 Samuel 19.5 Ecclésiaste 4.5 Psaumes 119.109
15 Tazama, ataniua; sina tumaini; ila hata hivyonitaithibitisha njia yangu mbele yake.
Proverbes 14.32 Job 27.5 Job 23.10 Psaumes 23.4 Job 40.8
16 Hili nalo litakuwa ni wokovu wangu; Kwani asiyemcha Mungu hatakaribia mbele yake.
Esaïe 12.1-12.2 Job 8.13 Jérémie 3.23 Exode 15.2 Actes 13.47
17 Sikieni sana maneno yangu, Maelezo yangu na yaingie masikioni mwenu.
Job 21.2 Job 33.1 Job 13.6
18 Angalieni sasa, nimekwisha kulitengeneza neno langu, Najua ya kuwa ni mwenye haki mimi.
Job 23.4 Job 9.2-9.3 Esaïe 43.26 Romains 8.33-8.34 Job 16.21
19 Yuko nani atakayeshindana nami? Maana sasa nitanyamaa kimya na kutoa roho.
Esaïe 50.7-50.8 Job 19.5 Job 10.8 Job 33.5-33.7 Romains 8.33
20 Lakini msinifanyie mambo mawili, hayo tu, Ndipo nami sitajificha usoni pako;
Genèse 3.8-3.10 Apocalypse 6.15-6.16 Psaumes 139.12 Job 9.34-9.35
21 Uondoe mkono wako usinilemee; Na utisho wako usinitie hofu.
Job 33.7 Job 9.34 Psaumes 39.10 Job 13.11 Job 10.20
22 Basi uite wakati huo, nami nitaitika; Au, niache ninene mimi, nawe unijibu.
Job 14.15 Job 42.3-42.6 Job 40.4-40.5 Job 9.16 Job 9.32
23 Maovu yangu na dhambi zangu ni ngapi? Nijulishe kosa langu na dhambi yangu.
Job 36.8-36.9 Job 22.5 Psaumes 139.23 Psaumes 44.20-44.21
24 Mbona umeuficha uso wako, Na kunihesabu kuwa ni adui yako?
Job 19.11 Lamentations 2.5 Psaumes 13.1 Job 33.10 Esaïe 8.17
25 Je! Utalitaabisha jani lipeperushwalo? Au, je! Utayafuatia hayo mabua makavu?
Job 21.18 Lévitique 26.36 Job 14.3 Matthieu 12.20 1 Samuel 24.14
26 Kwani umeandika maneno ya uchungu juu yangu, Na kunirithisha maovu ya ujana wangu;
Psaumes 25.7 Jean 5.5 Psaumes 88.3-88.18 Jean 5.14 Jérémie 31.19
27 Waitia miguu yangu katika mkatale, na kuyaaua mapito yangu yote; Wajiandikia alama kuzizunguka nyayo za miguu yangu;
Job 33.11 Job 2.7 2 Chroniques 16.10-16.12 Job 10.6 Job 14.16
28 Nijapokuwa ni kama kitu kilichooza, kinachosinyaa, Mfano wa nguo iliyoliwa na nondo.
Job 4.19 Psaumes 39.11 Nombres 12.12 Osée 5.12 Job 30.29-30.30

Cette Bible est dans le domaine public.