Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Esaïe 32
Bible en Swahili de l’est


1 Tazama, mfalme atamiliki kwa haki, na wakuu watatawala kwa hukumu.
Jérémie 33.15 Esaïe 9.6-9.7 Apocalypse 19.11 2 Chroniques 31.20-31.21 Esaïe 11.4
2 Na mwanadamu atakuwa kama mahali pa kujificha na upepo, na mahali pa kujisitiri na dhoruba; kama mito ya maji mahali pakavu, kama kivuli cha mwamba mkubwa katika nchi yenye uchovu.
Esaïe 25.4 Esaïe 9.6 Esaïe 44.3 Esaïe 7.14 Zacharie 13.7
3 Tena macho yao waonao hayatakuwa na kiwi, na masikio yao wasikiao yatasikiliza.
Esaïe 29.18 Marc 8.22-8.25 Matthieu 13.11 Actes 26.18 Esaïe 30.26
4 Tena moyo wa mtu mwenye hamaki utafahamu maarifa, na ndimi zao wenye kigugumizi zitakuwa tayari kunena sawasawa.
Esaïe 29.24 Matthieu 16.17 Exode 4.11 Néhémie 8.8-8.12 Actes 2.4-2.12
5 Mpumbavu hataitwa tena mwungwana, wala ayari hatasemwa kwamba ni karimu.
Esaïe 5.20 Psaumes 15.4 Malachie 3.18 1 Samuel 25.3-25.8 1 Samuel 25.25
6 Maana mpumbavu atanena yaliyo upumbavu, na moyo wake utafanya maovu, ili kutenda hila na kusema yasiyo kweli juu ya Bwana, ili kuziacha nafsi za watu wenye njaa hazina kitu, na kukikomesha kinywaji chake mwenye kiu.
Esaïe 3.15 1 Samuel 24.13 Matthieu 15.19 Matthieu 12.34-12.36 Jérémie 13.23
7 Tena vyombo vyake ayari ni vibaya; hutunga hila mbaya, ili kuwaangamiza wanyonge kwa maneno ya uongo, mtu mhitaji ajaposema maneno yenye haki.
Jérémie 5.26-5.28 Esaïe 5.23 Esaïe 61.1 Psaumes 82.2-82.5 1 Rois 21.10-21.14
8 Bali mwungwana huwaza mambo ya kiungwana, naye hushika sana mambo ya kiungwana.
Actes 9.39 Actes 11.29-11.30 2 Corinthiens 9.6-9.11 2 Corinthiens 8.2 Luc 6.33-6.35
9 Inukeni, enyi wanawake wenye raha, isikieni sauti yangu; enyi binti za watu msiokuwa na uangalifu, tegeni masikio yenu msikie matamko yangu.
Esaïe 28.23 Esaïe 3.16 Juges 9.7 Matthieu 13.9 Amos 6.1-6.6
10 Maana mtataabishwa siku kadha wa kadha zaidi ya mwaka, enyi wanawake mliojikinai; kwa sababu mavuno ya mizabibu yatakoma, wakati wa kuvuna vitu vya mashamba hautakuja.
Esaïe 7.23 Jérémie 8.13 Joël 1.12 Sophonie 1.13 Esaïe 16.10
11 Tetemekeni, enyi wanawake wenye raha; taabikeni, enyi msiokuwa na uangalifu; jivueni, jivueni nguo zenu kabisa, jivikeni viuno nguo za magunia.
Esaïe 33.14 Esaïe 3.24 Jacques 5.5 Deutéronome 28.48 Esaïe 47.1-47.3
12 Watajipiga vifua kwa ajili ya mashamba mazuri, kwa ajili ya mzabibu uliozaa sana.
Nahum 2.7 Deutéronome 8.7-8.8 Lamentations 4.3-4.4 Deutéronome 11.11-11.12 Ezéchiel 20.15
13 Juu ya nchi ya watu wangu itamea michongoma na mibigili; naam, juu ya nyumba za furaha katika mji ulio na shangwe;
Esaïe 22.2 Esaïe 34.13 Esaïe 7.23 Osée 9.6 Jérémie 39.8
14 maana jumba la mfalme litaachwa; mji uliokuwa na watu wengi utakuwa hauna mtu; kilima na mnara utakuwa makao ya wanyama milele, furaha ya punda-mwitu, malisho ya makundi ya kondoo;
Esaïe 25.2 Esaïe 27.10 Esaïe 24.12 Esaïe 24.10 Esaïe 5.9
15 hata roho itakapomwagwa juu yetu kutoka juu; hata jangwa litakapokuwa shamba lizaalo sana; nalo shamba lizaalo sana litakapohesabiwa kuwa msitu.
Esaïe 29.17 Ezéchiel 39.29 Esaïe 35.1-35.2 Tite 3.5-3.6 Esaïe 44.3
16 Ndipo hukumu itakaa katika jangwa, na haki itakaa katika shamba lizaalo sana.
Tite 2.11-2.12 1 Pierre 4.1-4.4 1 Corinthiens 6.9-6.11 Esaïe 35.8 Osée 3.5
17 Na kazi ya haki itakuwa amani; na mazao ya haki yatakuwa ni utulivu na matumaini daima.
Psaumes 119.165 Psaumes 85.8 Romains 14.17 Philippiens 4.6-4.9 Esaïe 26.3
18 Na watu wangu watakaa katika kao la amani; na katika maskani zilizo salama, na katika mahali pa kupumzikia penye utulivu.
Osée 2.18-2.23 Esaïe 60.17-60.18 Ezéchiel 34.25-34.26 Zacharie 2.5 Esaïe 35.9-35.10
19 Lakini mvua ya mawe itakunya, wakati wa kuangushwa miti ya msituni; na huo mji utadhilika.
Esaïe 28.17 Esaïe 30.30 Esaïe 28.2 Esaïe 26.5 Zacharie 11.2
20 Heri ninyi mpandao mbegu kando ya maji yote, na kuiacha miguu ya ng’ombe na punda waende ko kote.
Ecclésiaste 11.1 Esaïe 30.23-30.24 Actes 2.41 1 Corinthiens 9.9-9.11 Actes 4.4

Cette Bible est dans le domaine public.