Appel à suivre l’exemple de Paul
1 Hatimaye, ndugu zangu, furahini katika Bwana. Kuwaandikieni mambo yale yale hakuniudhi mimi, bali kutawafaa ninyi.
Philippiens 4.4 1 Pierre 4.13 2 Corinthiens 13.11 1 Thessaloniciens 5.16 Philippiens 4.8
2 Jihadharini na mbwa, jihadharini na watendao mabaya, jihadharini na wajikatao.
2 Corinthiens 11.13 Galates 5.15 Psaumes 22.20 Apocalypse 22.15 Psaumes 22.16
3 Maana sisi tu tohara, tumwabuduo Mungu kwa Roho, na kuona fahari juu ya Kristo Yesu, wala hatuutumainii mwili.
Colossiens 2.11 Galates 6.13-6.15 Romains 2.25-2.29 Deutéronome 30.6 Romains 4.11-4.12
4 Walakini mimi ningeweza kuutumainia mwili. Mtu ye yote akijiona kuwa anayo sababu ya kuutumainia mwili, mimi zaidi.
2 Corinthiens 11.18-11.22
5 Nalitahiriwa siku ya nane, ni mtu wa taifa la Israeli, wa kabila ya Benyamini, Mwebrania wa Waebrania, kwa habari ya kuishika torati, ni Farisayo,
2 Corinthiens 11.22 Romains 11.1 Actes 23.6 Actes 22.3 Genèse 17.12
6 kwa habari ya juhudi, mwenye kuliudhi Kanisa, kwa habari ya haki ipatikanayo kwa sheria sikuwa na hatia.
Actes 8.3 Actes 22.3-22.4 Galates 1.13-1.14 Actes 26.9-26.10 Actes 9.1-9.19
7 Lakini mambo yale yaliyokuwa faida kwangu, naliyahesabu kuwa hasara kwa ajili ya Kristo.
Luc 14.33 Proverbes 13.8 Luc 14.26 Matthieu 16.26 Proverbes 23.23
8 Naam, zaidi ya hayo, nayahesabu mambo yote kuwa hasara kwa ajili ya uzuri usio na kiasi wa kumjua Kristo Yesu, Bwana wangu; ambaye kwa ajili yake nimepata hasara ya mambo yote nikiyahesabu kuwa kama mavi ili nipate Kristo;
2 Pierre 1.3 Jean 17.3 Actes 20.24 Philippiens 3.10 Jérémie 9.23-9.24
9 tena nionekane katika yeye, nisiwe na haki yangu mwenyewe ipatikanayo kwa sheria, bali ile ipatikanayo kwa imani iliyo katika Kristo, haki ile itokayo kwa Mungu, kwa imani;
1 Corinthiens 1.30 Romains 8.1 2 Corinthiens 5.21 Philippiens 3.6 Esaïe 53.11
10 ili nimjue yeye, na uweza wa kufufuka kwake, na ushirika wa mateso yake, nikifananishwa na kufa kwake;
Romains 8.17 Galates 2.20 Romains 6.3-6.11 Philippiens 3.8 2 Timothée 2.11-2.12
11 ili nipate kwa njia yo yote kuifikia kiyama ya wafu.
Apocalypse 20.5 Luc 20.35-20.36 Actes 26.7 Hébreux 11.35 2 Thessaloniciens 2.3
12 Si kwamba nimekwisha kufika, au nimekwisha kuwa mkamilifu; la! Bali nakaza mwendo ili nipate kulishika lile ambalo kwa ajili yake nimeshikwa na Kristo Yesu.
1 Timothée 6.11-6.12 Osée 6.3 1 Timothée 6.19 Philippiens 3.13-3.14 Ephésiens 1.4
13 Ndugu, sijidhanii nafsi yangu kwamba nimekwisha kushika; ila natenda neno moja tu; nikiyasahau yaliyo nyuma, nikiyachuchumilia yaliyo mbele;
Luc 9.62 Hébreux 12.1-12.2 Hébreux 6.1 Philippiens 3.12 Philippiens 3.8
14 nakaza mwendo, niifikilie mede ya thawabu ya mwito mkuu wa Mungu katika Kristo Yesu.
1 Corinthiens 9.24 1 Pierre 5.10 Apocalypse 3.21 2 Corinthiens 4.17-5.1 2 Pierre 1.3
15 Basi sisi tulio wakamilifu na tuwaze hayo; na hata mkiwaza mengine katika jambo lo lote, Mungu atawafunulia hilo nalo.
Galates 5.10 1 Corinthiens 2.6 Proverbes 2.3-2.6 Luc 11.13 Proverbes 3.5-3.6
16 Lakini, hapo tulipofika na tuenende katika lilo hilo.
Galates 6.16 Apocalypse 3.3 Colossiens 2.6 Apocalypse 2.4-2.5 Romains 12.16
17 Ndugu zangu, mnifuate mimi, mkawatazame wao waendao kwa kuufuata mfano tuliowapa ninyi.
1 Pierre 5.3 Philippiens 4.9 1 Corinthiens 4.16 Romains 16.17 1 Thessaloniciens 2.10-2.14
18 Maana wengi huenenda, ambao nimewaambieni mara nyingi habari zao, na sasa nawaambia hata kwa machozi, kuwa ni adui za msalaba wa Kristo;
Galates 1.7 Galates 6.12 Jérémie 13.17 Ephésiens 4.17 Galates 2.14
19 mwisho wao ni uharibifu, mungu wao ni tumbo, utukufu wao u katika fedheha yao, waniao mambo ya duniani.
Romains 16.18 2 Pierre 2.3 Romains 8.5-8.7 2 Corinthiens 11.15 2 Pierre 2.1
20 Kwa maana sisi, wenyeji wetu uko mbinguni; kutoka huko tena tunamtazamia Mwokozi, Bwana Yesu Kristo;
Ephésiens 2.19 Hébreux 12.22 Colossiens 3.1-3.3 2 Corinthiens 4.18-5.1 Ephésiens 2.6
21 atakayeubadili mwili wetu wa unyonge, upate kufanana na mwili wake wa utukufu, kwa uweza ule ambao kwa huo aweza hata kuvitiisha vitu vyote viwe chini yake.Colossiens 3.4 1 Corinthiens 15.42-15.56 1 Jean 3.2 Ephésiens 1.19-1.20 Osée 13.14