Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Rois 17
Bible en Swahili de l’est


1 Basi Eliya Mtishbi, wa wageni wa Gileadi, akamwambia Ahabu, Kama Bwana, Mungu wa Israeli, aishivyo, ambaye ninasimama mbele zake, hakutakuwa na umande wala mvua miaka hii, ila kwa neno langu. Jacques 5.17 Luc 1.17 1 Rois 22.14 2 Rois 3.14 Luc 4.25-4.26
2 Neno la Bwana likamjia, kusema, 1 Rois 12.22 Osée 1.1-1.2 Jérémie 7.1 Jérémie 11.1 Jérémie 18.1
3 Ondoka hapa, geuka, uende upande wa mashariki, ujifiche karibu na kijito cha Kerithi kinachokabili Yordani. Apocalypse 12.6 Psaumes 83.3 Jean 8.59 Actes 17.14 Jérémie 36.19
4 Itakuwa utakunywa maji ya kile kijito; nami nimewaamuru kunguru wakulishe huko. Psaumes 147.9 1 Rois 17.9 1 Rois 19.5-19.8 Job 34.29 Nombres 20.8
5 Basi akaenda akafanya kama alivyosema Bwana; kwa kuwa akaenda akakaa karibu na kijito cha Kerithi, kinachokabili Yordani. Matthieu 16.24 Proverbes 3.5 Jean 15.14 1 Rois 19.9
6 Kunguru wakamletea mkate na nyama asubuhi, na mkate na nyama jioni, akanywa maji ya kile kijito. Exode 16.35 Hébreux 6.18 Habakuk 3.17-3.18 Psaumes 37.3 Luc 22.35
7 Ikawa, baada ya siku kupita, kile kijito kikakatika, kwa sababu mvua haikunyesha katika nchi. Esaïe 54.10 Esaïe 40.30-40.31
8 Neno la Bwana likamjia, kusema, Hébreux 13.6 Genèse 22.14 Esaïe 41.17 1 Rois 17.2
9 Ondoka, uende Sarepta, ulio mji wa Sidoni, ukae huko. Tazama, nimemwagiza mwanamke mjane wa huko akulishe. Abdias 1.20 Luc 4.26 1 Rois 17.4 Juges 7.4 Matthieu 15.21-15.22
10 Basi, akaondoka, akaenda Sarepta; hata alipofika langoni pa mji, kumbe! Mwanamke mjane alikuwako akiokota kuni; akamwita, akamwambia, Niletee, nakuomba, maji kidogo chomboni nipate kunywa. Jean 4.7 Genèse 24.17 2 Corinthiens 11.27 Hébreux 11.37 Genèse 21.15
11 Alipokuwa akienda kuleta, akamwita akasema, Niletee, nakuomba, kipande cha mkate mkononi mwako. Genèse 24.18-24.19 Hébreux 13.2 Matthieu 25.35-25.40 Genèse 18.5 1 Rois 17.9
12 Naye akasema, Kama Bwana, Mungu wako, aishivyo, sina mkate, ila konzi ya unga katika pipa, na mafuta kidogo katika chupa; nami ninaokota kuni mbili ili niingie nijipikie nafsi yangu na mwanangu, tuule tukafe. 1 Rois 17.1 2 Rois 4.2-4.7 Genèse 21.16 1 Samuel 26.10 Joël 1.15-1.16
13 Eliya akamwambia, Usiogope; enenda ukafanye kama ulivyosema; lakini unifanyie kwanza mkate mdogo ukaniletee; kisha ujifanyie nafsi yako na mwanao. Esaïe 41.13 Actes 27.24 Matthieu 6.33 Esaïe 41.10 Exode 14.13
14 Kwa kuwa Bwana, Mungu wa Israeli, asema hivi, Lile pipa la unga halitapunguka, wala ile chupa ya mafuta haitaisha, hata siku ile Bwana atakapoleta mvua juu ya nchi. 2 Rois 3.16 Matthieu 14.17-14.20 2 Rois 7.1 1 Rois 17.4 2 Rois 4.42-4.44
15 Basi akaenda, akafanya kama alivyosema Eliya; na yeye mwenyewe, na Eliya, na nyumba yake, wakala siku nyingi. Genèse 6.22 Jean 11.40 2 Chroniques 20.20 Genèse 12.4 Hébreux 11.7-11.8
16 Lile pipa la unga halikupunguka, wala ile chupa ya mafuta haikuisha, sawasawa na neno la Bwana alilolinena kwa kinywa cha Eliya. Luc 1.45 Luc 1.37 Matthieu 9.28-9.30 1 Rois 16.12 Jean 4.50-4.51
17 Ikawa, baada ya hayo, mwana wake yule mwanamke, bibi wa nyumba ile, akaugua; ugonjwa wake ukazidi hata akawa hana pumzi tena. Job 34.14 Jean 11.14 Jacques 1.12 Jean 11.3-11.4 Psaumes 104.29
18 Akamwambia Eliya, Nina nini nawe, Ee mtu wa Mungu? Je! Umenijia ili dhambi yangu ikumbukwe, ukamwue mwanangu? 2 Rois 3.13 Luc 5.8 Luc 4.34 Jean 2.4 2 Samuel 16.10
19 Akamwambia, Nipe mwanao. Akamtoa katika kifua chake, akamchukua juu chumbani mle alimokaa mwenyewe, akamlaza kitandani pake. 2 Rois 4.32 2 Rois 4.10 2 Rois 4.21 Actes 9.37
20 Akamwomba Bwana, akanena, Ee Bwana, Mungu wangu, je! Umemtenda mabaya mjane huyu ninayekaa kwake hata kumfisha mwanawe. 2 Rois 19.15 Jacques 5.15-5.18 Psaumes 73.13-73.14 Genèse 18.23-18.25 1 Rois 18.36-18.37
21 Akajinyosha juu ya mtoto mara tatu, akamwomba Bwana, akanena, Ee Bwana, Mungu wangu, nakusihi, roho ya mtoto huyu imrudie ndani yake tena. Actes 20.10 Actes 9.40 2 Rois 4.33-4.35 Hébreux 11.19 Actes 10.10
22 Bwana akaisikia sauti ya Eliya; na roho ya mtoto ikamrudia, akafufuka. 1 Samuel 2.6 Hébreux 11.35 Luc 8.54 Deutéronome 32.39 Jean 11.43
23 Eliya akamtwaa mtoto, akamchukua toka orofani mpaka chini ya nyumba ile, akampa mama yake. Eliya akanena, Tazama, mwanao yu hai. 2 Rois 4.36-4.37 Luc 7.15 Hébreux 11.35 Actes 9.41
24 Mwanamke akamwambia Eliya, Sasa najua ya kuwa wewe ndiwe mtu wa Mungu, na ya kuwa neno la Bwana kinywani mwako ni kweli. Jean 3.2 Jean 16.30 Jean 2.11 Jean 11.15 Jean 15.24

Cette Bible est dans le domaine public.