Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 102.6
Bible en Swahili de l’est


Prière dans la détresse

1 Ee Bwana, usikie kuomba kwangu, Kilio changu kikufikie.
Psaumes 61.2 Exode 2.23 Psaumes 18.6 Lamentations 3.18-3.20 Lamentations 3.44
2 Usinifiche uso wako siku ya shida yangu, Unitegee sikio lako, siku niitapo unijibu upesi.
Psaumes 69.17 Psaumes 27.9 Psaumes 88.2-88.18 Psaumes 71.2 1 Corinthiens 10.13
3 Maana siku zangu zinatoweka kama moshi, Na mifupa yangu inateketea kama kinga.
Jacques 4.14 Lamentations 1.13 Job 30.30 Psaumes 37.20 Psaumes 31.10
4 Moyo wangu umepigwa kama majani na kukauka, Naam, ninasahau kula chakula changu.
Psaumes 37.2 Esaïe 40.7 Esdras 10.6 Psaumes 77.3 Actes 9.9
5 Kwa ajili ya sauti ya kuugua kwangu Mifupa yangu imegandamana na nyama yangu.
Job 19.20 Proverbes 17.22 Lamentations 4.8 Psaumes 6.8 Psaumes 6.6
6 Nimekuwa kama mwari nyuni wa jangwani, Na kufanana na bundi wa mahameni.
Sophonie 2.14 Apocalypse 18.2 Esaïe 38.14 Job 30.29-30.30 Michée 1.8
7 Nakesha, tena nimekuwa kama shomoro Aliye peke yake juu ya nyumba.
Psaumes 77.4 Psaumes 38.11 Psaumes 22.2 Psaumes 130.6 Marc 14.33-14.37
8 Adui zangu wananilaumu mchana kutwa; Wanaonichukia kana kwamba wana wazimu Huapa kwa kunitaja mimi.
Actes 26.11 Esaïe 65.15 Luc 6.11 Psaumes 31.11-31.13 Psaumes 89.51
9 Maana nimekula majivu kama chakula, Na kukichanganya kinywaji changu na machozi.
Psaumes 42.3 Psaumes 80.5 Psaumes 69.21 Michée 7.17 Esaïe 44.20
10 Kwa sababu ya ghadhabu yako na hasira yako; Maana umeniinua na kunitupilia mbali.
Psaumes 38.3 Psaumes 147.6 Lamentations 1.18 Lamentations 5.16 Psaumes 39.11
11 Siku zangu zi kama kivuli kilichotandaa, Nami ninanyauka kama majani.
Job 14.2 Psaumes 109.23 Psaumes 144.4 Psaumes 102.3-102.4 Psaumes 39.5-39.6
12 Bali Wewe, Bwana utaketi ukimiliki milele, Na kumbukumbu lako kizazi hata kizazi.
Psaumes 135.13 Psaumes 9.7 Exode 3.15 Lamentations 5.19 Deutéronome 33.27
13 Wewe mwenyewe utasimama, Na kuirehemu Sayuni, Kwa maana ndio wakati wa kuihurumia, Naam, majira yaliyoamriwa yamewadia.
Galates 4.4 Psaumes 44.26 Esaïe 40.2 2 Pierre 3.8 2 Pierre 3.12
14 Maana watumishi wako wameyaridhia mawe yake, Na kuyaonea huruma mavumbi yake.
Néhémie 4.2 Néhémie 4.10 Néhémie 2.17 Psaumes 137.5-137.6 Daniel 9.16
15 Kisha mataifa wataliogopa jina la Bwana, Na wafalme wote wa dunia utukufu wako;
Psaumes 138.4 1 Rois 8.43 Psaumes 68.31-68.32 Esaïe 60.3-60.22 Esaïe 55.5
16 Bwana atakapokuwa ameijenga Sayuni, Atakapoonekana katika utukufu wake,
Esaïe 60.1-60.2 Psaumes 147.2 Psaumes 69.35 Esaïe 66.18 Jérémie 31.4
17 Atakapoyaelekea maombi yake aliye mkiwa, Asiyadharau maombi yao.
Néhémie 1.6 Psaumes 22.24 Jérémie 29.11-29.14 Daniel 9.3-9.21 Psaumes 9.18
18 Kizazi kitakachokuja kitaandikiwa hayo, Na watu watakaoumbwa watamsifu Bwana.
Romains 15.4 1 Corinthiens 10.11 Psaumes 22.30-22.31 Esaïe 43.21 Exode 17.14
19 Maana ametazama toka patakatifu pake pa juu, Toka mbinguni Bwana ameiangalia nchi,
Deutéronome 26.15 Psaumes 14.2 1 Rois 8.39 Hébreux 9.23-9.24 2 Chroniques 16.9
20 Ili akusikie kuugua kwake aliyefungwa, Na kuwafungua walioandikiwa kufa.
Psaumes 79.11 Psaumes 146.7 Ephésiens 2.2-2.3 Esaïe 61.1-61.3 Esaïe 14.17
21 Watu walitangaze jina la Bwana katika Sayuni, Na sifa zake katika Yerusalemu,
Psaumes 22.22 1 Pierre 2.9 Ephésiens 3.21 Psaumes 9.13-9.14 Ephésiens 2.4-2.7
22 Pindi mataifa watapokusanyika pamoja, Falme nazo ili kumtumikia Bwana.
Zacharie 8.20-8.23 Esaïe 49.22-49.23 Matthieu 24.14 Psaumes 72.8-72.11 Psaumes 22.27
23 Amezipunguza nguvu zangu njiani; Amezifupisha siku zangu.
2 Thessaloniciens 2.3-2.12 2 Timothée 3.1-3.17 Apocalypse 11.2-11.19 Apocalypse 12.13-12.17 1 Timothée 4.1-4.3
24 Nitasema, Ee Mungu wangu, usiniondoe katikati ya siku zangu; Miaka yako ni tangu kizazi hata kizazi.
Habakuk 1.12 Psaumes 102.12 Psaumes 39.13 Apocalypse 1.8 Psaumes 90.1-90.2
25 Hapo mwanzo uliutia msingi wa nchi, Na mbingu ni kazi ya mikono yako.
Genèse 1.1 Hébreux 1.10-1.12 Genèse 2.1 Psaumes 96.5 Job 38.4-38.7
26 Hizi zitaharibika, bali Wewe utadumu Naam, hizi zitachakaa kama nguo; Na kama mavazi utazibadilisha, Nazo zitabadilika.
Esaïe 34.4 Esaïe 51.6 Apocalypse 20.11 Matthieu 24.35 Apocalypse 21.1
27 Lakini Wewe U Yeye yule; Na miaka yako haitakoma.
Malachie 3.6 Jacques 1.17 Hébreux 13.8 Apocalypse 1.17-1.18 Jean 8.58
28 Wana wa watumishi wako watakaa, Na wazao wao wataimarishwa mbele zako.
Psaumes 45.16-45.17 Psaumes 69.35-69.36 Esaïe 66.22 Esaïe 65.22 Esaïe 53.10

Cette Bible est dans le domaine public.