Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Philippiens 2.10
Bible en Swahili de l’est


1 Basi ikiwako faraja yo yote katika Kristo, yakiwako matulizo yo yote ya mapenzi, ukiwako ushirika wo wote wa Roho, ikiwako huruma yo yote na rehema,Colossiens 3.12 1 Jean 4.12 2 Corinthiens 13.14 Psaumes 133.1 1 Jean 4.7-4.8
2 ijalizeni furaha yangu, ili mwe na nia moja, wenye mapenzi mamoja, wenye roho moja, mkinia mamoja.Romains 12.16 1 Corinthiens 1.10 1 Pierre 3.8-3.9 2 Corinthiens 13.11 Jean 3.29
3 Msitende neno lo lote kwa kushindana wala kwa majivuno; bali kwa unyenyekevu, kila mtu na amhesabu mwenziwe kuwa bora kuliko nafsi yake.Romains 12.10 Ephésiens 4.2 Ephésiens 5.21 Galates 5.26 1 Pierre 5.5
4 Kila mtu asiangalie mambo yake mwenyewe, bali kila mtu aangalie mambo ya wengine.1 Corinthiens 10.24 Romains 15.1 Jacques 2.8 Matthieu 18.6 1 Corinthiens 10.32-10.33
5 Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu;Matthieu 11.29 1 Jean 2.6 1 Pierre 2.21 1 Pierre 4.1 1 Corinthiens 10.33-11.1
6 ambaye yeye mwanzo alikuwa yuna namna ya Mungu, naye hakuona kule kuwa sawa na Mungu kuwa ni kitu cha kushikamana nacho;Hébreux 1.3 Jean 5.18 Apocalypse 21.6 2 Corinthiens 4.4 Hébreux 13.8
7 bali alijifanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa wanadamu;2 Corinthiens 8.9 Matthieu 20.28 Jean 1.14 Galates 4.4 Romains 8.3
8 tena, alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam, mauti ya msalaba.Hébreux 12.2 Jean 10.18 Matthieu 26.39 Romains 5.19 2 Corinthiens 8.9
9 Kwa hiyo tena Mungu alimwadhimisha mno, akamkirimia Jina lile lipitalo kila jina;Matthieu 28.18 Hébreux 2.9 1 Pierre 3.22 Esaïe 52.13 Psaumes 110.5
10 ili kwa jina la Yesu kila goti lipigwe, la vitu vya mbinguni, na vya duniani, na vya chini ya nchi;Esaïe 45.23-45.25 Matthieu 28.18 Hébreux 1.6 Apocalypse 5.13-5.14 Jean 5.28-5.29
11 na kila ulimi ukiri ya kuwa YESU KRISTO NI Bwana, kwa utukufu wa Mungu Baba.Jean 13.13 Romains 14.9 1 Jean 4.15 Psaumes 110.1 1 Corinthiens 12.3
12 Basi, wapendwa wangu, kama vile mlivyotii sikuzote, si wakati mimi nilipokuwapo tu, bali sasa zaidi sana mimi nisipokuwapo, utimizeni wokovu wenu wenyewe kwa kuogopa na kutetemeka.2 Pierre 1.5-1.10 1 Corinthiens 15.58 Luc 13.23-13.24 Philippiens 3.13-3.14 1 Pierre 2.11
13 Kwa maana ndiye Mungu atendaye kazi ndani yenu, kutaka kwenu na kutenda kwenu, kwa kulitimiza kusudi lake jema.Hébreux 13.21 2 Corinthiens 3.5 2 Timothée 1.9 Ephésiens 1.5 Ephésiens 2.8
14 Yatendeni mambo yote pasipo manung’uniko wala mashindano,1 Pierre 4.9 1 Corinthiens 10.10 Proverbes 13.10 Jacques 1.20 Matthieu 20.11
15 mpate kuwa wana wa Mungu wasio na lawama, wala udanganyifu, wasio na ila kati ya kizazi chenye ukaidi, kilichopotoka; ambao kati ya hao mnaonekana kuwa kama mianga katika ulimwengu,Matthieu 5.14-5.16 Matthieu 5.45 1 Pierre 2.12 Tite 2.10 Deutéronome 32.5
16 mkishika neno la uzima; nipate sababu ya kuona fahari katika siku ya Kristo, ya kuwa sikupiga mbio bure wala sikujitaabisha bure.Galates 2.2 2 Corinthiens 1.14 1 Thessaloniciens 2.19 1 Jean 1.1 1 Thessaloniciens 3.5
17 Naam, hata nikimiminwa juu ya dhabihu na ibada ya imani yenu, nafurahi; tena nafurahi pamoja nanyi nyote.2 Timothée 4.6 2 Corinthiens 12.15 Romains 15.16 Colossiens 1.24 Philippiens 1.20
18 Nanyi vivyo hivyo furahini, tena furahini pamoja nami.Jacques 1.2-1.4 Philippiens 4.4 Philippiens 3.1 Ephésiens 3.13
19 Walakini natumaini katika Bwana Yesu kumtuma Timotheo afike kwenu karibu, nifarijiwe na mimi, nikiijua hali yenu.Philippiens 1.1 1 Corinthiens 4.17 1 Thessaloniciens 3.2 2 Timothée 1.12 Jérémie 17.5
20 Maana sina mtu mwingine mwenye nia moja nami, atakayeiangalia hali yenu kweli kweli.1 Corinthiens 16.10 Philippiens 2.2 Psaumes 55.13 2 Timothée 1.5 1 Timothée 1.2
21 Maana wote wanatafuta vyao wenyewe, sivyo vya Kristo Yesu.1 Corinthiens 10.24 1 Corinthiens 13.5 2 Timothée 3.2 Philippiens 2.4 Esaïe 56.11
22 Ila mwajua sifa yake, ya kuwa ametumika pamoja nami kwa ajili ya Injili, kama mwana na baba yake.1 Corinthiens 4.17 1 Timothée 1.2 2 Timothée 1.2 2 Corinthiens 2.9 Actes 16.3-16.12
23 Basi, natumaini kumtuma huyo mara, hapo nitakapojua yatakayonipata.1 Samuel 22.3 Philippiens 2.19
24 Nami naamini katika Bwana ya kuwa nitakuja na mimi mwenyewe hivi karibu.Philémon 1.22 Philippiens 2.19 3 Jean 1.14 Philippiens 1.25-1.26 2 Jean 1.12
25 Lakini naliona imenilazimu kumtuma kwenu Epafrodito, ndugu yangu, mtenda kazi pamoja nami, askari pamoja nami; tena ni mtume wenu na mhudumu wa mahitaji yangu.Philippiens 4.18 Philémon 1.1-1.2 Philippiens 4.3 Philémon 1.24 2 Timothée 2.3-2.4
26 Kwa kuwa alikuwa na shauku kwenu ninyi nyote, akahuzunika sana, kwa sababu mlisikia ya kwamba alikuwa hawezi.Romains 12.15 Philippiens 1.8 1 Corinthiens 12.26 Psaumes 69.20 Philippiens 1.3
27 Kwa maana alikuwa hawezi kweli kweli, karibu na kufa; lakini Mungu alimhurumia; wala si yeye peke yake, ila na mimi pia; nisiwe na huzuni juu ya huzuni.Habakuk 3.2 Psaumes 34.19 Jérémie 8.18 Actes 9.39-9.41 Esaïe 27.8
28 Kwa hiyo nimefanya bidii nyingi zaidi kumtuma, ili mtakapomwona tena mpate kufurahi, nami nipunguziwe huzuni yangu.1 Jean 1.3-1.4 Actes 20.38 Genèse 45.27-45.28 2 Corinthiens 2.3 Philippiens 2.26-2.27
29 Mpokeeni, basi, katika Bwana, kwa furaha yote, mkawahesabu watu kama huyu kuwa watu wa kuheshimiwa.1 Corinthiens 16.18 Romains 16.2 1 Timothée 5.17 1 Thessaloniciens 5.12 Actes 28.10
30 Maana kwa ajili ya kazi ya Kristo alikaribia kufa akaponza roho yake; ili kusudi ayatimize yaliyopungua katika huduma yenu kwangu.1 Corinthiens 16.17 Actes 20.24 Philippiens 4.10 Apocalypse 12.11 1 Corinthiens 16.10

Cette Bible est dans le domaine public.