16 Bwana akamwambia Musa, Mwambie Haruni, Nyosha fimbo yako, ukayapige mavumbi ya nchi, ili kwamba yawe chawa katika nchi yote ya Misri. Exode 8.17 Exode 8.5 17 Nao wakafanya; Haruni akaunyosha mkono wake na fimbo yake, na kuyapiga mavumbi ya nchi, nayo yakawa chawa juu ya wanadamu na juu ya wanyama; mavumbi yote ya nchi yakawa ni chawa katika nchi yote ya Misri. Psaumes 105.31 Actes 12.23 Esaïe 23.9 18 Hao waganga nao wakafanya mfano wa hayo kwa uganga wao, ili kwamba walete chawa, lakini wasiweze; nako kulikuwa na chawa juu ya wanadamu, na juu ya wanyama. Exode 7.11 Exode 9.11 Daniel 5.8 Esaïe 47.12-47.13 Esaïe 19.12 19 Ndipo wale waganga wakamwambia Farao, Jambo hili ni chanda cha Mungu; na moyo wake Farao ukawa mgumu asiwasikize; vile vile kama Bwana alivyonena. Psaumes 8.3 Luc 11.20 Actes 4.16 Matthieu 12.28 Daniel 2.19 20 Bwana akamwambia Musa, Inuka asubuhi na mapema usimame mbele ya Farao; angalia! Atoka aende majini; kamwambie, Bwana asema, Wape watu wangu ruhusa waende zao, ili wanitumikie mimi. Exode 7.15 Exode 8.1 Exode 9.13 Exode 3.18 21 Au kwamba huwapi ruhusa watu wangu, tazama, nitaleta wingi wa mainzi juu yako wewe, na juu ya watumishi wako, na juu ya watu wako, nao wataingia ndani ya nyumba zako; na nyumba za Wamisri zitajawa na wingi wa mainzi, na nchi nayo ambayo wa juu yake. Esaïe 7.18 Psaumes 78.45 Psaumes 105.31 22 Nami siku hiyo nitatenga nchi ya Gosheni, watu wangu wanayokaa, ili hao mainzi wasiwe huko; ili kwamba upate kujua wewe ya kuwa mimi ndimi Bwana kati ya dunia. Exode 9.4 Malachie 3.18 Exode 9.6 Exode 10.23 Exode 9.26 23 Nami nitatia mpaka kati ya watu wangu na watu wako; ishara hiyo italetwa kesho. 24 Bwana akafanya; wakaja wingi wa mainzi kwa uzito sana, wakaingia nyumbani mwa Farao, na katika nyumba za watumishi wake, tena katika nchi yote ya Misri; nayo nchi iliharibiwa kwa ajili ya wale mainzi. Psaumes 105.31 Psaumes 78.45 Exode 8.21 25 Farao akawaita Musa na Haruni akawaambia, Endeni mkamtolee Mungu wenu dhabihu ndani ya nchi hii. Exode 9.27 Exode 8.8 Exode 10.16 Exode 12.31 Apocalypse 3.9 26 Musa akasema, Haitupasi kufanya hivyo; kwa kuwa tutamchinjia sadaka Bwana, Mungu wetu, na hayo machukizo ya Wamisri; je! Tutachinja sadaka ya hayo machukizo ya Wamisri mbele ya macho yao, wasitupige kwa mawe? Genèse 43.32 Genèse 46.34 2 Corinthiens 6.14-6.17 Esdras 9.1 Exode 3.18 27 La, tutakwenda safari ya siku tatu jangwani, tumchinjie dhabihu Bwana, Mungu wetu, kama atakavyotuagiza. Exode 3.18 Exode 3.12 Lévitique 10.1 Exode 34.11 Exode 5.1 28 Farao akasema, Mimi nitawapa ruhusa mwende, ili mmchinjie dhabihu Bwana, Mungu wenu, jangwani; lakini hamtakwenda mbali sana; haya niombeeni. Exode 8.8 1 Rois 13.6 Exode 9.28 Exode 8.29 Esdras 6.10 29 Musa akasema, Tazama, mimi natoka kwako, nami nitamwomba Bwana ili hao mainzi wamtoke Farao, na watumishi wake, na watu wake kesho; lakini Farao asitende kwa udanganyifu tena, kwa kutowaacha watu waende kumchinjia Bwana dhabihu. Exode 8.15 Jérémie 42.20-42.21 Exode 8.8 Psaumes 66.3 Psaumes 78.34-78.37 30 Musa akatoka kwa Farao, akamwomba Bwana. Exode 8.12 Jacques 5.16 Exode 9.33 31 Bwana akafanya kama neno la Musa, akawaondoa wale mainzi wabaya kwake Farao, na kwa watumishi wake, na watu wake; hakusalia hata mmoja. 32 Farao akaufanya moyo wake kuwa mzito mara hiyo nayo, wala hakuwapa ruhusa hao watu waende zao. Exode 8.15 Exode 4.21 Romains 2.5 Exode 7.13-7.14 Jacques 1.13-1.14